Friday, October 5, 2012

Mkutano wa Cheetah Development

Jana jioni nilihudhuria shughuli ya Cheetah Development mjini St. Paul. Cheetah Development ni mtandao wa watu wanaojishughulisha na miradi ya maendeleo Afrika Mashariki, hasa Tanzania. Nilijulishwa kuhusu mtandao huu na rafiki yangu Mzee Paul Bolstad, ambaye anaonekana kushoto kabisa hapa pichani.
Yeye na huyu mwingine ni marafiki wa tangu zamani. Wote ni wapenzi wakubwa wa Tanzania. Mzee Bolstad alizaliwa na kukulia Tanzania, na huyu mwenzake walikuwa wote katika programu ya Peace Corps Tanzania walipokuwa vijana.
Walihudhuria watu wengi Kulikuwa na hotuba na maonesho ya shughuli mbali mbali za Cheetah Development.





































Kikundi cha kwaya kiitwacho imuka, kutoka Bukoba, ambacho kiko katika ziara hapa Marekani, kilitoa burudani.













Tulikutana wa-Tanzania kadhaa, tukabadilisha mawazo na kupiga michapo.

No comments:

Tangazo la Maongezi Yangu Books on Central, Faribault

Kwa miaka mingi, nimeongea na hadhira mbali mbali hasa kuhusu tofauti za tamaduni. Matangazo huandaliwa na kusambazwaa kabla ya mikutano. Ka...