
Nilipokuwa Johannesburg, mwezi Juni, nilitembelea sehemu kadhaa za jiji hilo. Hiyo ilikuwa ni tarehe 17. Kwenye kitongoji cha Newton niliweza kuona taasisi kadhaa, mojawapo ikiwa
Museum Africa. Hili ni jumba la makumbusho ambamo wamehifadhi vitu vingi vya kihistoria. Kwa mfano, kuna picha nyingi sana na maelezo kuhusu siku za mwanzo kabisa za Johannesburg, kwa mfano usafiri ulivyokuwa, simu, nyumba ya mwanzo ya ibada, na idara ya mwanzo kabisa ya zimamoto, ambayo haikuwa na vifaa tunavyovijua leo. Ni kumbukumbu murua sana kwa yeyote anayeithamini historia.
Museum Africa sio kumbukumbu pekee eneo hili la Newton. Ziko nyingine pia. Ukiingia humo ukakaa saa moja, mbili, au zaidi ukiangalia na kusoma yaliyomo, utatoka ukiwa umeelimika sana. Insh'Allah nitaleta taarifa zaidi.
No comments:
Post a Comment