Rachel na Anna waliniomba nikawe mwanajopo katika mjadala wa leo, kwa vile wanafahamu ninafahamika na kukubalika katika jamii ile. Mjadala ulilenga kuwapa fursa wazazi na vijana kufahamu hali halisi, faida na changamoto za vyuo kwa wa-Islam ambao pia ni wahamiaji kutoka Afrika.
Sunday, October 30, 2011
Wa-Islamu Vyuoni Marekani
Rachel na Anna waliniomba nikawe mwanajopo katika mjadala wa leo, kwa vile wanafahamu ninafahamika na kukubalika katika jamii ile. Mjadala ulilenga kuwapa fursa wazazi na vijana kufahamu hali halisi, faida na changamoto za vyuo kwa wa-Islam ambao pia ni wahamiaji kutoka Afrika.
Saturday, October 29, 2011
Wednesday, October 26, 2011
Mwandishi Nuruddin Farah Katutembelea


Miaka ya hivi karibuni, hapa chuoni St. Olaf, nimefundisha pia riwaya zingine za Nuruddin Farah. Ni mmoja wa waandishi bora kabisa kutoka Afrika, ambaye ameshapata tuzo nyingi kwa uandishi wake.
Tuesday, October 25, 2011
Vitabu Vyangu Vinapatikana Bagamoyo
Mmiliki ni Dada Neema, mjasiriamali anayeuza vitu mbali mbali, kuanzia vinyago, vikapu, na nguo za ki-Tanzania, hadi picha na postikadi za ki-Tanzania.
Nilionana naye hapa Bagamoyo mwaka jana, na ndipo alipofahamu habari za vitabu vyangu, akaamua awe anaviuza, kama wanavyofanya wajasiriamali wengine wawili watatu nchini Tanzania. Mimi si mfanyabiashara bali mwalimu na mwandishi. Ila niko tayari muda wote kuwawezesha wajasiriamali kuvipata vitabu vyangu. Namba ya simu ya duka la Dada Neema ni 0754 445 956.
Sunday, October 23, 2011
Taswira za Mjini Songea
Nchi yetu ya Tanzania ni kubwa sana. Ina mikoa, wilaya na vijiji vingi, na siamini kama yuko m-Tanzania atakayeweza kupita kila sehemu. Mimi mwenyewe nimebahatika kutembelea sehemu nyingi katika mikoa mbali mbali. Hata hivyo, kuna sehemu ambazo sijafika, kama vile Bukoba, Mpanda, Sumbawanga, na Singida.
Kutokana na ukweli huo, ninawashukuru wanablogu ambao wamekuwa mstari wa mbele kutuletea habari na taarifa za sehemu mbali mbali za nchi yetu. Blogu ya Mwenyekiti Mjengwa ilinigusa kwa namna ya pekee tangu mwanzo, kwa jinsi alivyokuwa anatembelea vijiji ambavyo wengi wetu hatutavifikia. Kutokana na jinsi nilivyofaidika na jambo hilo, nami najaribu kuleta picha za sehemu mbali mbali, ili wa-Tanzania wengine wapate kuzifahamu sehemu ambako nimefika.
Leo naleta baadhi ya picha nilizopiga mjini Songea mwaka huu. Nimeshaleta taarifa kadhaa za Songea katika blogu hii, kama vile hii hapa. Napangia kuleta taarifa na picha zaidi. Wale ambao hawajafika Songea watapata fununu kidogo kuhusu mahali hapo, ingawa picha zote ni za sehemu ya katikati ya mji.







Kutokana na ukweli huo, ninawashukuru wanablogu ambao wamekuwa mstari wa mbele kutuletea habari na taarifa za sehemu mbali mbali za nchi yetu. Blogu ya Mwenyekiti Mjengwa ilinigusa kwa namna ya pekee tangu mwanzo, kwa jinsi alivyokuwa anatembelea vijiji ambavyo wengi wetu hatutavifikia. Kutokana na jinsi nilivyofaidika na jambo hilo, nami najaribu kuleta picha za sehemu mbali mbali, ili wa-Tanzania wengine wapate kuzifahamu sehemu ambako nimefika.
Leo naleta baadhi ya picha nilizopiga mjini Songea mwaka huu. Nimeshaleta taarifa kadhaa za Songea katika blogu hii, kama vile hii hapa. Napangia kuleta taarifa na picha zaidi. Wale ambao hawajafika Songea watapata fununu kidogo kuhusu mahali hapo, ingawa picha zote ni za sehemu ya katikati ya mji.







Saturday, October 22, 2011
Ukiwa na Siri, Iweke Kitabuni
Hapa kuna picha nilizopiga kwenye tamasha la vitabu mjini Minneapolis, Oktoba 15, mwaka huu. Habari za tamasha hilo niliziandika hapa.
Picha zote hizi nilizipiga kwa muda wa dakika mbili hivi, nikiwa nimesimama sehemu moja.
Niliangalia jinsi watu walivyokuwa wanavichangamkia vitabu. Nilikumbuka ule usemi kuwa ukiwa na siri, iweke kitabuni. Hapo watu makini na wasio makini watajipambanua wenyewe.
Kwa uzoefu wangu, kama ninavyosema tena na tena katika blogu na sehemu zingine, wa-Marekani ni kati ya hao watu makini. Ukiweka siri kitabuni, wataiona.
Friday, October 21, 2011
Sehemu za Kupumzikia, Mbamba Bay
Mbamba Bay ni mji mdogo, kando kando ya Ziwa Nyasa, upande wa Tanzania. Ingawa umaarufu wa mji huu tangu zamani ni bandari, hapo ni mahali pazuri kwa mapumziko. Picha ninazoleta hapa nilipiga mwanzoni mwa Agosti, mwaka huu.
Unaweza kusogea hapo ufukweni, ukawa unapunga upepo na kuangalia shughuli za wavuvi, wauzaji wa samaki, akina mama wakifua nguo, na watoto wakicheza majini. Kama unajua kuogelea, mahali hapo utafafurahia. Ukija siku ambapo meli inakuja, utajionea ujio wa meli na kuondoka kwake.
Kama unapenda kukaa kwenye mwinuko, uangalie mji na Ziwa kwa chini yako, hoteli ya masista panafaa. Habari zake niliandika hapa. Ukipata chumba kinachoangalia upande wa Ziwa, huko nyuma ya hoteli, utafaidi mandhari ya Ziwa na sehemu kadhaa za Mbamba Bay. Ukitoka nje ukaingia bustanini, utapanda mawe na kuliona Ziwa vizuri sana.
Hapo kwenye paa la blue ni baa ya Four Ways, ambayo picha zake niliwahi kuziweka hapa. Mwaka huu, nilipokuwa Mbamba Bay sikupata fursa ya kuingia ndani.
Hapa kushoto niko katika baa ya Bush House na wadau niliokutana nao humo, ambao walitaka tupige picha.




Monday, October 17, 2011
Ziara ya Uyole Kufuatilia Chuo Kikuu Kipya
Binafsi, naunga mkono mipango ya kujenga vyuo vipya kama hiki cha Uyole. Kwanza, idadi ya waTanzania inaongezeka muda wote, na mahitaji ya vyuo hayatapungua. Ni vema kujenga sasa, kwa kadiri iwezekanavyo, kuliko kungoja hadi baadaye, wakati gharama zinaendelea kupanda.
Hata kama vyuo vitakuwa vingi mno na wanafunzi wasiwe wa kutosha, jambo la kuzingatia ni kuwa vyuo vyetu vikiwa bora sana vitawavutia wanafunzi na watafiti kutoka nchi za nje, kama ilivyokuwa kwa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam miaka ya zamani. Faida zake ni nyingi, kuanzia za kitaaluma, kwa maana ya fursa ya kubalishana mawazo baina ya watu wa mitazamo mbali mbali, hadi kiuchumi. Kwa mfano, Marekani inatambua jambo hilo, na inajivunia malaki ya wanafunzi wanaosoma katika nchi hiyo kutoka duniani kote. Pamoja na faida kubwa za kitaaluma, wageni hao wanaingiza mamilioni ya dola katika uchumi wa Marekani kila mwaka.
Ni muhimu kwa sisi wa-Tanzania kuwa na mawazo mapana kuhusu masuala ya aina hii. Tuwekeze katika vyuo pia, ila tuwe makini katika kuhimiza na kuboresha taaluma, utafiti, na maadili yahusikayo. Lakini kwa hali ilivyo, tuko nyuma sana. Baadhi ya wanaoongoza vyuo vyetu hawana upeo utakiwao, na serikali haina upeo huo. Serikali imekuwa na historia ya kuwapachika watu kwenye nafasi za uongozi wa vyuo bila kuzingatia masuala muhimu ya misingi, maana na wajibu wa vyuo vikuu. Kukosekana kwa upeo huu ni msingi mkubwa wa migomo na vurugu zisizoisha katika vyuo vyetu ambazo hukwamisha uwezo wa kuviweka vyuo vyetu katika viwango vitakiwavyo.
Sunday, October 16, 2011
JK na Pinda Wakiwapagawisha Wadau

Saturday, October 15, 2011
Tamasha la Vitabu, Minneapolis
Thursday, October 13, 2011
Ni Msimu Mwingine kwa Wanafiki Kumkumbuka Nyerere Kinafiki!

Chanzo Raia Mwema
Ni msimu mwingine kwa wanafiki kumkumbuka Nyerere kinafiki!
Johnson Mbwambo
12 Oct 2011
KESHOKUTWA, Ijumaa, Oktoba 14, Taifa litatimiza miaka 12 kamili tangu kifo cha Baba wa Taifa, Mwalimu Nyerere, kilichotokea kule London, Uingereza katika hospitali ya Mtakatifu Thomas.
Kama ambavyo imekuwa kwa miaka 11 iliyopita, Watanzania wataitumia pia keshokutwa kumkumbuka mpendwa wao huyo; huku wakitafakari, kama Taifa,
zile “t” tatu maarufu : Tulikotoka, tulipo na tunakokwenda.
Na kama ilivyokuwa kwa miaka 11 iliyopita, Taifa litaiadhimisha siku hiyo ya Ijumaa, Oktoba 14, kwa makongamano, semina na matamasha yenye mahusiano na maisha ya Baba wa Taifa.
Kama ilivyokuwa kwa miaka 11 iliyopita, maadhimisho hayo ya kumbukumbu ya Nyerere yatapambwa na kauli nzito kuhusu mchango wake katika kujenga Taifa letu, mawazo yake na visheni yake.
Wengi wataonyesha kwa dhati hisia zao za mapenzi waliyokuwanayo kwa mtu huyo ambaye, kwa jinsi alivyoipenda Tanzania, mimi naamini itatuchukua miaka 50 mingine kumpata anayemkaribia japo kwa asilimia 60 tu!
Lakini watakuwepo pia viongozi wachache wanafiki ambao watasimama majukwaani na, kwa unafiki, kuisifu visheni na uongozi wa Nyerere; huku kiutendaji wakiendelea kuibomoa misingi yote ya taifa ambayo mzee wetu huyo alitujengea.
Ndugu zangu, ni kipindi kama hiki ambapo tutawasikia hata wale waliokuwa wafuasi wake wakubwa katika kuitekeleza siasa ya Ujamaa na Kujitegemea katika Tanzania, lakini baadaye wakaitelekeza siasa hiyo, wakitoa kauli za kumsifu Mwalimu Nyerere kwa yale yote aliyoyasimamia. Ni Oktoba 14 ya kila mwaka wanapodhihirisha unafiki wao huo.
Ngoja tuwakumbushe unafiki wao viongozi hao wanafiki ambao zamani walikuwa wafuasi wa Nyerere, lakini sasa ni wafuasi wa Ubeberu wa Magharibi unaozidi kuwakamua wakulima na wafanyakazi masikini wa nchi hii.
Tuanze na Siasa ya Kujitegemea: Nyerere aliwaambia hivi kuhusu hilo, na wakajitia wako naye: “Tutaijenga nchi hii kwa faida yetu wenyewe. Akipatikana mtu wa kutusaidia, tutamshukuru. Lakini kazi ya kujenga nchi hii kwa manufaa ya Watanzania wote ni kazi ya Watanzania, si kazi ya mtu mwingine.”
Natujiulize; Baada ya kifo cha Mwalimu, Oktoba 14, 1999, wafuasi wake hao ambao bado wapo madarakani ndivyo wanavyoiendesha nchi? Je; wanaamini na kutekeleza dhana hiyo ya kujitegemea?
Jibu langu ni “hapana”. Angalau bado tunamkumbuka mtawala wa sasa (Rais Kikwete), kwenye kampeni za mwaka jana, alipoomba apewe kura kwa sababu yeye ni hodari wa “kuhemea vibaba Ughaibuni”.
Mtawala mwenye mtazamo huo hawezi kamwe kuwa muumini wa kweli wa Siasa ya Kujitegemea ambayo Mwalimu Nyerere alipigania kuijenga nchini wakati wote wa uhai wake.
Kwa hiyo, si siri kwamba watawala wetu wa sasa si waumini wa kweli wa dhana ya kujitegemea, na ndiyo maana safari zao kwenda Ughaibuni kutembeza bakuli la ombaomba zimekuwa nyingi tangu Mwalimu afariki. Majuzi tu hapa Kikwete karejea kutoka Marekani (kuhemea!?) na aliporejea, Waziri Mkuu wake, Mizengo Pinda naye akapanda ndege kwenda Brazil (kuhemea?!).
Vyovyote vile; kama wafuasi hawa wa zamani wa Mwalimu Nyerere watazungumza lolote la kumkumbuka hiyo Ijumaa, Oktoba 14, na kusema kuwa wanafuata nyayo zake katika suala hilo la kujitegemea, watakuwa wanadhalilisha uwezo wetu wa kufikiri, na kwa hakika, watakuwa wanauanika tu hadharani unafiki wao!
Kuhusu ujenzi wa Ujamaa na kuupiga vita Ubepari; wafuasi hao wa Mwalimu wanaonyesha unafiki huo huo. Si siri kwamba Ujamaa aliouhubiri Nyerere sasa umebaki kwenye Katiba tu; huku wakubwa wakiimba na kucheza ngoma ya Ubepari.
Haikuwachukua hata miaka saba tangu Nyerere aondoke madarakani kwa wafuasi wake hao kuliua Azimio la Arusha la mwaka 1967 kwa kuweka Azimio la Zanzibar mwaka 1992. Na bado Ijumaa, Oktoba 14, kina Ngombale Mwiru watakuwa na ujasiri wa kupanda jukwaani na kutoa kauli za kulisifu Azimio la Arusha alilolipigania Nyerere; ilhali ndio hao hao walioliua kwa azimio lile la Zanzibar!
Wafuasi hao wameliua Azimio la Arusha na Siasa ya Ujamaa na Kujitegemea na wakaamua kuukumbatia Ubepari, lakini sote tunajua jinsi Mwalimu alivyouchukia Ubepari (kiasi cha kuuita ni unyama). Alipata kusema hivi: “Ni majitu (mabepari) yanayokaa na uwezo wao na yanatumia wengine kama vyombo vya uzalishaji. Kwa hiyo, kwao mfanyakazi na randa ni sawa sawa. Nasema nchi ya namna hiyo inaitwa ni nchi ya kibepari.”
Katika suala la fursa sawa kwa wote, pia matendo yao hayaendani na ya Mwalimu. Enzi za Mwalimu, kila mwananchi alikuwa na fursa sawa, na haikujalisha utajiri au umasikini wake, kabila lake, elimu yake, dini yake au rangi yake.
Lakini tangu Mwalimu aondoke, mambo yamebadilika kwa kasi. Hivi sasa kuzungumzia fursa sawa kwa mtoto wa kiongozi (tajiri) na mtoto wa masikini, kunahitaji ujasiri wa ‘ki-uendawazimu’.
Hali imebadilika mno. Mfano mzuri ni katika elimu. Wakati watoto wa wakulima masikini wanakalia ndoo shuleni kwa sababu ya ukosefu wa madawati, watoto wa viongozi ama wanasoma nje ya nchi au katika shule za binafsi zenye kila kitu.
Hata katika suala la ujenzi wa uchumi wa viwanda nchini pia wameitelekeza visheni ya Mwalimu. Mwalimu alisema hivi kuhusu viwanda: “Maana ya maendeleo ya leo ya uchumi wenye nguvu, ni maendeleo ya viwanda. Nchi yenye viwanda tunasema ni nchi iliyoendelea. Nchi haiwezi kuendelea bila kuwa na viwanda vya kisasa.”
Ili kulitekeleza hilo kwa vitendo, Mwalimu alisimamia ujenzi wa viwanda vingi nchini. Kwa mfano, mpaka wakati anaondoka madarakani, nchi ilikuwa na viwanda vya nguo 12.
Lakini alipong’atuka madarakani, hao waliokuwa wafuasi wake wakaanza mbio za kuuza viwanda hivyo vya umma kwa watu binafsi; tena kwa bei ya kutupa. Ilikuwa ni katika kutekeleza sera yao mpya ya uchumi wa soko huria.
Matokeo yake ni kwamba hivi sasa ni kama vile sekta ya viwanda haipo kabisa katika Tanzania! Kutoka kwenye viwanda 12 vya nguo (kwa mfano) sasa nchi ina viwanda vitatu tu vya nguo! Leo hii, hata leso tu za kujifutia jasho zinatoka Beijing kwenye viwanda vya Wachina!
Pamoja na usaliti huo, bado watawala wetu watakuwa na ujasiri, hiyo Oktoba 14, kupanda jukwaani na kutudanganya kuwa wanaifuata sera ya Mwalimu ya ujenzi wa uchumi wa viwanda! Unafiki mtupu!
Hata katika suala la kudumisha amani na usalama ambao ndio umekuwa wimbo wao mkubwa siku hizi wa kuwatisha wapinzani, ni hivyo hivyo. Watasimama majukwaani na kutuongopea kwamba wanaijenga misingi iliyowekwa na Mwalimu ya kudumisha amani na usalama nchini!
Uongo mtupu; maana sote tunakumbuka kwamba Mwalimu alisema kuwa “usione vinaelea, vimeundwa”; kwamba amani tuliyonayo inatokana na misingi ya usawa iliyojengwa, na kwamba hatuwezi kubaki nayo kama tutaachia pengo kati walio nacho na wasio nacho liongezeke.
Kwa hali ilivyo hivi sasa, pengo hilo limekuwa kubwa mno. Wakati wanavijiji wengi nchini wanaishi katika nyumba za mbavu za mbwa, viongozi mijini wanamiliki majumba kadhaa ya kifahari.
Wakati masikini wanakula mlo mmoja kwa siku, matajiri wanakula na kusaza, na wakati Watanzania wengi wanashindwa kumudu kununua hata baiskeli moja tu, viongozi na matajiri wanamiliki misururu ya magari ya kifahari nk.
Mwalimu alipata kututahadharisha kuhusu hali hiyo kwa kusema hivi: “Wachache wanapoonekana waziwazi wakiogelea katika utajiri wa wizi na magendo na unyonyaji, wakati wengi wanakabiliana na dhiki ya kweli kweli, si rahisi kulinda amani na umoja wetu.
Je; watawala wetu wa sasa wanazingatia tahadhari hiyo ya Mwalimu kwamba tusiruhusu pengo kati ya matajiri na masikini liongezeke? Jibu unalo mwenyewe mpenzi msomaji.
Tukija kwenye suala la ardhi na maliasili zetu nyingine ni hivyo hivyo. Mwalimu alitambua na kuthamini haki ya wananchi kumiliki ardhi, lakini baada ya kifo chake sote tumeshuhudia ekari kwa ekari za ardhi za wananchi wakipewa wawekezaji. Hali hii imeibua misuguano mikubwa kati ya wananchi na wawekezaji hao huko Loliondo, Babati, Manyara na Mbarali.
Katika sekta ya madini, stori ni hizo hizo. Mwalimu hakuwa na pupa kubinafisha migodi yetu kwa wageni. Alitaka Watanzania wajiandae vyema kabla ya kuchimba migodi hiyo ili iweze kuwaletea maendeleo. Lakini alipokufa, sote tuliiona kasi ya kina Mkapa kuibinafsisha migodi hiyo kwa wawekezaji wa kigeni! Na sasa, muda si mrefu watatuachia mashimo matupu!
Ndugu zangu, ninaweza hata kuandika vitabu vitatu kueleza mambo mengi mema ambayo Mwalimu alituwekea misingi na kutuonyesha njia; lakini wale waliokuwa wafuasi wake wakaamua kuyatelekeza na kutuchagulia njia potevu baada ya kifo chake; lakini itoshe tu kusema kwamba laana yake itawashukia.
Nina hakika kama muujiza ungetendeka na Mwaliimu akafufuka leo, na kuyaona hayo yanayofanywa na waliokuwa wafuasi wake, angewakana mara moja kwa kusema: “Hakika, siwajua watu hawa waovu”.
Nihitimishe safu yangu kwa kukumbusha tena kwamba, huu ni msimu mwingine kwa viongozi wanafiki kumkumbuka Mwalimu Nyerere ki-nafiki. Kwa mwaka mwingine tena, watapanda majukwaani, Ijumaa, Oktoba 14 na kumpamba Nyerere na kusifia sera na miongozo yake; huku wakijua mioyoni mwao kwamba si waumini wa kweli wa fikra zake, na kwamba wanachokifanya ni kinyume kabisa na mafundisho yake.
Hata hivyo, unafiki huo wanaoufanya ni kwa madhara ya afya zao wenyewe! Niwakumbushe wanafiki hao maneno ya Yurii katika riwaya ya Doctor Zhivago ya mwandishi mahiri wa kale wa Urusi, Boris Pasternak.
Yurii anasema hivi: Your health is bound to be affected if day after day, you say the opposite of what you feel, if you grovel before what you dislike ”; yaani kwamba utaathirika kiafya iwapo siku hadi siku utazungumza kinyume ya kile unachokiamini.
Kama hivyo ndivyo, basi, nawashauri wanafiki hawa ambao zamani walikuwa wafuasi wa kweli wa Mwalimu Nyerere lakini wakayatosa mafundisho yake baada ya yeye kufariki; kuzijali, basi, afya zao na kuepuka hiyo Ijumaa, Oktoba 14, kuyasifia mafundisho yake na yale yote aliyoyasimamia wakati wa uhai wake; ilhali mioyoni mwao wanajua kwamba hawayaamini!
Ujumbe wangu kwao ni huu: Watakuwa wanazilinda afya zao kama watakuwa wakweli kuhusu waguswavyo na Nyerere. Waache unafiki.
Lakini kwa waumini wa kweli wa Mwalimu Nyerere, niwakumbushe tu kwamba wana kila sababu ya kusimama kijasiri majukwaani na kumtetea Mwalimu kwa nguvu zao zote; maana hata kama alifanya makosa ya hapa na pale, yake yalikuwa ni makosa ya kibinadamu.
Yake hayakuwa ni makosa yaliyochochewa na uchu wa kutajirika zaidi na zaidi katikati ya mamilioni ya watu masikini; kama ilivyo kwa watawala wetu wa sasa.
Nawatakieni nyote maadhimisho mema ya kumbukumbu ya miaka 12 ya kifo cha mpendwa wetu, J.K. Nyerere. Tafakari.
Wednesday, October 12, 2011
Maktaba ya Mkoa, Ruvuma

Napenda kuandika habari za maktaba za Tanzania. Nimeshaandika kuhusu maktaba ya Lushoto, Kilimanjaro, na Iringa. Nitaendelea kufanya hivyo.
Monday, October 10, 2011
Kitabu Kinapopigwa Marufuku
Tutafakari suala tata la kupiga marufuku vitabu. Sijui kama wewe mdau unaafiki suala la kitabu kupigwa marufuku. Mimi huwa nakerwa. Kwa kawaida, kitabu kikipigwa marufuku, huwa nakitafuta ili nikisome. Nimeelezea mtazamo wangu kuhusu suala hili kinaganaga katika kitabu cha CHANGAMOTO. Hapa naleta mifano miwili ya vitabu vilivyopigwa marufuku Tanzania.
Hapa kushoto ni kitabu cha Hamza Njozi kuhusu mauaji ya Mwembechai. Wako ambao waliona ni muhimu kitabu hiki kupigwa marufuku. Lakini mimi nilikitetea kwa kila namna, hata Njozi mwenyewe amenishukuru katika kitabu chake kilichofuata.
Kitabu kingine ni Satanic Verses, cha Salman Rushdie. Wako ambao waliona ni muhimu kitabu hiki kupigwa marufuku. Ayatollah Khomeini wa Iran alitangaza fatwa juu ya Salman Rushdie, kwamba ni ruksa kumwua popote. Tangu mwanzo, watalaam wa dini ya ki-Islam sehemu mbali mbali za dunia walipishana mawazo kuhusu jambo hilo. Wako ambao waliafiki fatwa na wengine walipinga. Chuo Kikuu maarufu cha ki-Islam cha Al-Azhar kilisema asiuawe bali kwanza apate fursa ya kujitetea na kutubu.
Suali langu ni je, unaafiki suala la kitabu kupigwa marufuku? Halafu, kwa ujumla wa-Tanzania hawana utamaduni wa kusoma vitabu. Kuna maana gani kupiga marufuku vitabu Tanzania, wakati hata vikiwepo, watu hawavisomi, na huenda wasitambue kwamba vipo?
Kupiga marufuku vitabu Tanzania ni kuwapa wa-Tanzania umaarufu ambao hawastahili, kwamba ni wasomaji wa vitabu. Nimeongelea kirefu zaidi masuala hayo katika kitabu cha CHANGAMOTO.


Suali langu ni je, unaafiki suala la kitabu kupigwa marufuku? Halafu, kwa ujumla wa-Tanzania hawana utamaduni wa kusoma vitabu. Kuna maana gani kupiga marufuku vitabu Tanzania, wakati hata vikiwepo, watu hawavisomi, na huenda wasitambue kwamba vipo?
Kupiga marufuku vitabu Tanzania ni kuwapa wa-Tanzania umaarufu ambao hawastahili, kwamba ni wasomaji wa vitabu. Nimeongelea kirefu zaidi masuala hayo katika kitabu cha CHANGAMOTO.
Saturday, October 8, 2011
Mkutano wa wa-Afrika na wa-Marekani Weusi Umefana
Aliongelea mengi, akasisitiza umuhimu wa kufahamiana kikweli kweli sio kijuu juu, ili kila mmoja aelewe mahitaji, mategemeo, na mataizo ya mwingine, ndipo tuweze kujenga mahusiano na mtandao wa kutupeleka mbele. Tuwe na moyo na kusaidiana, na hii ni pamoja na kusaidiana kuelimisha watoto wetu wote.
Msichana huyu mdogo alionyesha kipaji chake cha kucheza kwa kufuatilia muziki wa waimbaji fulani. Anatumia miondoko ambayo kwa ujumla inafanana na "ballet" ila niliona yeye anatumia zaidi ubunifu wake mwenyewe. Ni binti mahiri na alishangiliwa sana.
Subscribe to:
Posts (Atom)
Tangazo la Maongezi Yangu Books on Central, Faribault
Kwa miaka mingi, nimeongea na hadhira mbali mbali hasa kuhusu tofauti za tamaduni. Matangazo huandaliwa na kusambazwaa kabla ya mikutano. Ka...

-
Leo ni kumbukumbu ya siku ya kuzaliwa kwangu, ambayo ni tarehe 17 Agosti, 1951. Familia yangu, ndugu, na marafiki wamejumuika nami kushereh...
-
Leo napenda kukitambulisha kwako mdau kitabu muhimu cha ki-Swahili, Tenzi Tatu za Kale . Nilinunua nakala yangu miaka kadhaa iliyopita katik...
-
Kutafsiri kazi ya fasihi ni kazi ngumu ya kuchemsha bongo. Inahitaji ufahamu wa hali ya juu wa lugha husika, na pia hisia makini za kifasih...