

Lakini miaka ile mimi nilikuwa sijishughulishi sana na ki-Swahili. Nilizama katika maandishi ya ki-Ingereza. Vijana wenzangu waliopenda riwaya za ki-Ingereza walikuwa wanapenda sana riwaya kama za Ian Fleming na James Hadley Chase. Mimi sikuwahi kuzisoma hizo.
Nikirudi kwenye uandishi wa ki-Swahili, napenda kusema kuwa nashukuru kuwa miaka iliyofuata, nilijirudi, kama ninavyoelezea katika kitabu cha CHANGAMOTO: Insha za Jamii. Nami sasa nimejiunga na wasomaji wanaowaenzi waandishi wetu wanaotumia ki-Swahili.
Faraji Katalambula aliandika pia riwaya zingine, akaingia pia katika tasnia ya filamu. Ametoa mchango mkubwa kwa jamii, na ingawa ameondoka, kama walivyoondoka akina Mgeni bin Faqihi, Shaaban Robert, Amri Abedi, na Mathias Mnyampala, mchango wake utadumu duniani. Apumzike kwa amani.
No comments:
Post a Comment