Wednesday, February 22, 2012

Nilivyoanza Kupeleka Wanafunzi Tanzania

Nimetoka mbali, katika suala la kuwapeleka Tanzania wanafunzi wa vyuo vya Marekani. Mara baada ya kuja kufundisha katika Chuo Cha St. Olaf, nilianza kujishughulisha na masuala ya programu zinazowapeleka wanafunzi Afrika. Kama mmoja wa washauri wa programu hizo nilijifunza mengi. Baada ya miaka michache, nilianza kuwapeleka wanafunzi Tanzania.

Hapa kushoto niko na wanafunzi kwenye chuo kilichokuwa kinaitwa Danish, eneo la Usa River. Hii ilikuwa ni programu ya vyuo vilivyomo katika mtandao wa LCCT. Nadhani hiyo ilikuwa ni mwaka 1997. Hapo Danish, tulikuwa tunawapa wanafunzi mafunzo kuhusu masuala mbali mbali ya Tanzania, kwa wiki moja na kidogo. Baada ya hapo, kwa mujibu wa programu hii, niliwapeleka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, kusoma kwa muhula mmoja.



Hapa kushoto niko na wanafunzi wale wale katika nyumba niiyokuwa naishi pale Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, sehemu iitwayo "Research Flats."

Kadiri miaka ilivyopita, nimejijengea uzoefu na ufahamu mkubwa wa programu hizi. Nafahamu mikakati, mahitaji, changamoto, na faida za programu hizo kwa wahusika wa pande zote. Uzoefu wa kuwaandaa wanafunzi wa ki-Marekani kuishi katika utamaduni wa kigeni uliniwezesha kuandika kitabu kiitwacho Africans and Americans: Embracing Cultural Differences. Nilikiandika mahsusi kuchangia programu hizo, na walimu wengine wanaopeleka wanafunzi Afrika wanakitumia, bila kuwataja watu wanaoenda Afrika kwa utalii, shughuli za kujitolea, na kadhalika.

No comments:

Tangazo la Maongezi Yangu Books on Central, Faribault

Kwa miaka mingi, nimeongea na hadhira mbali mbali hasa kuhusu tofauti za tamaduni. Matangazo huandaliwa na kusambazwaa kabla ya mikutano. Ka...