
Hapa kushoto ni picha iliyopigwa Dar es Salaam mwaka 2004, wakati wa maonesho ya vitabu kwenye viwanja vya kumbukumbu za Taifa. Niko na dada yangu na wadau wa Canada, waliokuwa wanaishi Tanzania. Wakati ule nilikuwa nimechapisha vitabu viwili tu: Matengo Folktales na Notes on Achebe's Things Fall Apart.
Hao akina mama walipita kwenye meza yangu, wakaviangalia vitabu, halafu wakasema watapita tena baadaye kununua kitabu cha Matengo Folktales. Baada ya kusema hivyo, waliendelea na mizunguko yao katika vibanda vingine. Kwa kawaida, watu wakipita namna hii, huwa si rahisi kukumbuka kurudi tena. Lakini hao, baada ya muda mrefu, walirudi, wakanunua kitabu na tukapiga hiyo picha.


Hatimaye alikisoma kitabu cha Africans and Americans: Embracing Cultural Differences." Ana michapo mikali kuhusu jinsi mambo yalivyokuwa wakati anakisoma kitabu hicho. Mara kwa mara ananikumbuka, kwa simu au katika ukumbi wa Facebook.
Ndoto ya mwandishi ni kuona maandishi yake yanasomwa. Nami nawashukuru wadau hao, na wengine wote ambao siwajui.
No comments:
Post a Comment