Baada ya kuwa nao Tanzania kwa wiki tatu, niliwaacha Chuo Kikuu Dar es Salaam, ambapo walisoma kwa muhula moja, kwa mujibu wa programu. Wakisharejea Marekani, wanapata fursa ya kuongelea safari yao, masomo waliyosoma, na maisha yao Tanzania kwa ujumla.
Wanapokuwa Chuo Kikuu Dar, wanafunzi hao wa LCCT wanapata fursa ya kujitolea kama waalimu wasaidizi katika shule ya msingi ya Mlimani. Mwezi Agosti mwaka jana, nilipoenda hapo shule ya msingi kutoa taarifa kuhusu ujio wa wanafunzi hao, walimu walisema mpango huu wa wanafunzi wa ki-Marekani kujitolea pale una manufaa. Kwa mfano, watoto wanapata fursa ya kuboresha ufahamu wao wa ki-Ingereza.
Napenda kumalizia kwa kusema kuwa shughuli za kuendesha programu hizi ni za kujitolea. Hivi vikao vyetu, ambavyo vinadumu siku moja nzima na vinaendelea kwa nusu siku ifuatayo, ni vya kujitolea. Hapa Marekani sijaona utamaduni wa posho za vikao kama ilivyo Tanzania. Mnaletewa chakula, saa ifikapo, lakini sijawahi kuona wala kusikia kuhusu vibahasha kama Tanzania. Nimeona niseme hivyo, ili kuonyesha tofauti ilivyo, na papo hapo, hapa Marekani kazi inafanywa kwa roho moja.
No comments:
Post a Comment