Wednesday, May 20, 2015

Kitabu cha Honwana Kimefika Leo

Leo nina furaha sana. Nimepata kitabu cha Luis Bernardo Honwana, We Killed Mangy Dog and Other Stories, ambacho nilikiagiza siku chache zilizopita.

Hiki ni kitabu ambacho nimekuwa ninakikumbuka kwa namna ya pekee, tangu miaka ya mwanzoni kabisa ya sabini na kitu nilipokisoma kwa mara ya kwanza. Furaha iliyoje kuzikumbuka enzi zile za ujana wangu, nilipokuwa tayari nimetekwa moyo na akili na somo la fasihi ya ki-Ingereza.

Ingawa wakati huu ninapoandika, na kwa siku chache zijazo, niko katika kusahihisha mitihani, nitaanza kukisoma kitabu hiki mara. Siwezi kujizuia. Hatimaye, nitaandika uchambuzi mfupi katika blogu hii.

Kama nilivyosema kabla, kitabu hiki, kutoka Msumbiji, kitakuwa ni kianzio kwa ajili ya kufundisha riwaya ya Mia Couto, The Tuner of Silences, wakati wa kiangazi.

No comments:

Tangazo la Maongezi Yangu Books on Central, Faribault

Kwa miaka mingi, nimeongea na hadhira mbali mbali hasa kuhusu tofauti za tamaduni. Matangazo huandaliwa na kusambazwaa kabla ya mikutano. Ka...