.jpg)
Kimoja ni Uhuru Street, mkusanyo wa hadithi za kubuniwa,ambazo zinatokea katika mtaa wa Uhuru, mjini Dar es Salaam. Nasikitika kuwa kitabu hiki sijakisoma ingawa nimetamani kukisoma kwa miaka mingi. Kutokana na taarifa, nilijua kuwa kwa yeyote anayeijua Dar es Salaam, hiki ni kitabu kinachogusa hisia. Nimeanza kukisoma na ninajionea mwenyewe ukweli huo.
Kitabu cha pili ambacho kimewasili ni The Book of Secrets, ambacho, kama nilivyosema, niliwahi kukifundisha katika semina ya walimu katika Chuo cha Colorado. Mtu akisoma kitabu hiki, naamini atapata hamu ya kusoma vitabu vingine vya Moyez Vassanji.
Kitabu cha tatu ambacho kimewasili ni The In-Between World of Vikram Lall. Sijaanza kukisoma, ila nimekuwa nikisoma habari zake.
Kitabu kingine nilichokitaja siku chache zilizopita ni Amriika, ambacho nilikinunua zamani kidogo, ila sijakisoma. Moyez Vassanji ameshaandika vitabu karibu kumi hadi sasa. Ambavyo sijavitaja ni The Assasin's Song, No New Land, The Magic of Saida, A Place Within, na And Home Was Kariakoo. Orodha haiishii hapo, na kuvisoma vyote itakuwa kazi kubwa. Kwa vyo vyote, baadhi nitavitumia katika kozi yangu ya Post-colonial Literature.
.png)
Ninakiri kuwa si jambo la kuridhisha kwamba vitabu vingi vilivyovitaja hapo juu ambavyo vilichapishwa miaka iliyopita, sikuvisoma na bado sijavisoma. Hiyo ni dosari. Ninapaswa kumfahamu mwandishi kama Moyez Vassanji kama ninavyowafahamu waandishi ninaowasoma katika ki-Ingereza kama Wole Soyinka, Nadine Gordimer, Derek Walcott, J.M. Coetzee, Anita Desai, Athol Fugard, Ngugi wa Thiong'o, Chinua Achebe, Sembene Ousmane, Salman Rushdie, na kadhalika.
Panapo majaliwa, nitaandika katika blogu hii juu ya Abdulrazak Gurnah na Tololwa Mollel, ambao ni waandishi wengine maarufu wa ki-Tanzania huku ughaibuni wanaoandika kwa ki-Ingereza. Tuwe nao bega kwa bega. Ni aibu kwetu kwamba waandishi hao wanasifika nchi za ng'ambo lakini si nyumbani Tanzania.
No comments:
Post a Comment