Jiwe la Mmbuji

Hili ni Jiwe la Mmbuji. Liko mahali paitwapo Ngwambo, katika nchi ya Umatengo, wilayani Mbinga, mashariki ya Ziwa Nyasa. Jiwe hili kubwa linasemekana lina maajabu. Wamatengo tangu zamani wanasimulia mambo ya ajabu yanayotokea hapa. Wamatengo wanaamini kuna viumbe viitwavyo ibuuta . Ni kama binadamu, ila wadogo sana, na wa ajabu, na katika mataifa mengine wanajulikana pia, kwa majina mbali mbali. Wamatengo wanasema kuwa ibuuta wanakuwepo kwenye jiwe hili usiku wakifanya mambo yao. Nyumbani kwangu sio mbali na hapo, na jiwe hili tulikuwa tunalisikia tangu tukiwa wadogo. Tukipanda mlimani kijijini kwetu, tulikuwa tunaliona. Mwaka jana nilipita karibu na eneo hili, nikapiga picha ya jiwe hili kama inavyoonekana hapa. Hii ilikuwa ni mara yangu ya kwanza kulikaribia jiwe hili namna hii. Nilishangaa kuona watu wamelima mashamba karibu yake, na wanaishi sio mbali na hapo. Habari nilizozisikia tangu utoto wangu kuhusu jiwe hili zilinifanya niamini kuwa hakuna mtu anaweza kusogea hapo, achil