Monday, April 25, 2022

Mdau Wangu Makini Katutembelea

Leo hapa Chuoni St. Olaf alifika mama mmoja kutoka Togo ambaye anaishi kwenye mji wa mbali kiasi kutoka hapa nilipo. Alimleta binti yake kwenye programu fulani ya wanafunzi. 

Mama huyu ni mdau wangu hodari, kwa maana kwamba ni msomaji wa tangu zamani wa vitabu vyangu na maandishi mengine, na ni mfuatiliaji wa shughuli zangu za kuelimisha jamii. 

Kwenye haya matamasha, huwa sikosi kuwaona waAfrika  wa nchi kama vile Somalia,  Kenya, Ethiopia, Uganda, Sudani, Congo, Nigeria, Togo, Liberia au Ghana. Ninafurahi kuwa wadau kutoka nchi zote hizo wamenunua na wamevutiwa na kitabu changu kiitwacho Africans and Americans: Embracing Cultural Differences.



Tangazo la Maongezi Yangu Books on Central, Faribault

Kwa miaka mingi, nimeongea na hadhira mbali mbali hasa kuhusu tofauti za tamaduni. Matangazo huandaliwa na kusambazwaa kabla ya mikutano. Ka...