Saturday, February 12, 2022

MTanzania Ughaibuni Aongelea Kitabu cha "Matengo Folktales"

 

Wiki za hivi karibuni nimepata kufahamiana na dada Corona Cormak, mTanzania aishiye Jamhuri ya Czech. Ni mwandishi mahiri wa vitabu vya watoto, ambavyo nimesoma nikavifurahia. Pia ni msimuliaji hodari wa hadithi.

Wiki hii, katika ukurasa wake wa Instagram, Coriona ameandika uchambuzi wake wa kitabu changu Matengo Folktales. Ameandika hivi:

I will start with a big smile. This book Matengo Folktales by John Mbele @africonexion. Took me way back into those days of story telling. Three stories in this book were so vividly. The Monster in the Rice, The Tale of two women and the Tale of Katigija. The sound of the songs in these stories is what I am still trying to remember. These songs were always sang with everyone when the stories were narrated. This is what is missing in story telling these days. We let our children just listen to the story without them taking part.

However, I am quite shocked with the amount of killing in every story. At least I don't remember the killing part. For example the Tale of two women, I remember this part when the woman was told to lick the wounds. And in Katigija Tale I remember the grandma singing when she brought the food to the child and the Monster in the Rice field, I remember how the children kept on disappearing.

My son was shocked when I told him The tale of Monster in the Rice. He was like, what a story, what a family 🙈🤣
Beautiful written and I like the comment section. This helps one to understand why these stories were what they were.
Now I need someone to sing those songs for me 🥳🤗
 
Tafsiri ya juu juu ya kiSwahili ni hivi:

Nitaanza na tabasamu kubwa. Kitabu ni "Matengo Folktales" cha [Joseph] Mbele. Kilinirudisha kwenye siku zile za usimuliaji hadithi. Hadithi tatu katika kitabu hiki zilisisimua: “Jitu Katika Shamba la Mpunga,” “Kisa cha Wanawake Wawili” na "Hadithi ya Katigija.” Najaribu kukumbuka sauti za nyimbo katika hadithi zile. Nyimbo hizi daima ziliimbwa na wote wakati hadithi zinasimuliwa. Hicho ndicho kinachokosekana katika usimulizi wa hadithi leo. Tunawafanya watoto wetu wasikilize tu bila wao kushiriki.

Lakini, nimeshtushwa na idadi ya mauaji katika kila hadithi. Sikumbuki sawasawa sehemu ambapo mauaji yenyewe yanatokea. Kwa mfano, "Kisa cha Wanawake Wawili," nakumbuka pale mwanamke anapoambiwa kulamba vidonds. Na katika “Hadithi ya Katigija” nakumbuka bibi anavyoimba wakati anamletea mtoto Katigija chakula, na katika “Jitu Katika Shamba la Mpunga” nakumbuka jinsi watoto walivyokuwa wanapotea. Mtoto wangu alishtuka nilipomsimulia “Kisa cha Jitu Katika Shamba la Mpunga.” Alishangaa ni hadithi gani hiyo, na ni familia gani hiyo.
 
Kitabu kimeandikwa vizuri na nilipendezwa na maelezo kuhusu hadithi. Yanasaidia kuelewa kwa nini hadithi ziko zilivyo. Sasa nahitaji mtu wa kuniimbia nyimbo zilozomo.

 

 

Wednesday, February 9, 2022

Vitabu Viko Chuoni Mbeya

 

Tarehe 27 hadi 29 Januari, 2022, nilikuwa mgeni wa Catholic University College of Mbeya. Nilikuwa nimealikwa kutoa mhadhara juu ya “Africans and Americans: Embracing Cultural Differences.” Lakini nilijikuta katika shughuli zingine pia, ikiwemo mazungumzo na waalimu na pia mkuu wa chu

 

Katika mhadhara wangu, niliibua masuala ambayo nimeyaongelea katika vitabu vyangu Africans and Americans: Embracing Cultural Differences na Chickens in the Bus: More Thoughts on Cultural Differences. Lengo langu kuu lilikuwa kuanzisha jadi ya kutafakari changamoto za tofauti za tamaduni katika ulimwengu wa utandawazi wa leo.

Tafakari hii inapaswa iwe endelevu. Kuchangia hilo, nilikabidhi nakala za hivi vitabu vyangu viwili kwa ajili ya maktaba ya chuo. Baadaye mkurugenzi  wa maktaba ameniandikia ujumbe wa shukrani kwa kupewa vitabu hivyo. 

Tangazo la Maongezi Yangu Books on Central, Faribault

Kwa miaka mingi, nimeongea na hadhira mbali mbali hasa kuhusu tofauti za tamaduni. Matangazo huandaliwa na kusambazwaa kabla ya mikutano. Ka...