Mambo ya Tamasha la Vitabu Mankato

Kila tamasha la vitabu au utamaduni ninaloshiriki huwa na mambo mengi ya kuelimisha na kuburudisha akili. Kukutana na watu na kuongea nao ni sababu muhimu ya ushiriki wangu katika matamasha hayo. Juzi katika tamasha la Deep Valley Book Festival, binti yangu Zawadi nami, tunaoonekana pichani hapa kushoto, tulikutana na kuongea na watu mbali mbali. Kati ya hao alikuwepo mama mmoja ambaye si rahisi kumsahau. Alifika mezani petu, na wakati tunasalimiana alinyanyua nakala ya Matengo Folktales , Africans and Americans: Embracing Cultural Differences , Notes on Achebe's Things Fall Apart, na Africans in the World , akasema anavinunua. Wakati wote alikuwa anatuelezea kuwa alikuwa na binti yake ambaye aliishi China kwa miaka nane kisha akaenda Namibia, na kwamba ameipenda Namibia tangu mwanzo. Alituambia tumwekee vitabu vyake, na kwamba binti yake angefika baadaye. Yapata nusu saa kabla ya tamasha kwisha, huyu binti alikuja. Tuliongea naye, akatuambia jinsi alivyoipenda Namibi