Sunday, May 22, 2022

Huenda Nikaandika Kitabu Kingine Kuhusu Tamaduni

Tarehe 25 Agosti, 2021, nilichapisha kitabu, Chickens in the Bus: More Thoughts on Cultural Differe=-ians and Americans: Embracing Cultural Differences." Baada ya kuchapisha vitabu hivi, niliona sina haja ya kuandika kitabu kingine juu ya tamaduni.

Lakini, wiki kadhaa zilizopita, nilizindua programu ya mtandaoni, "Cross Cultural Conversations," ambayo naendesha kila Jumamosi. Ninaongea kupitia Zoom na kuwashirikisha wasikilizaji katika maongezi juu ya mada mbali mbali kuhusu tofauti baina utamaduni wa Afrika na wa Marekani.
Katika kufanya hivyo, nimejikuta nikizama zaidi katika masuala niliyoongelea katika vitabu vyangu, na ninaibua pia mengine au mitazamo ambayo haikuwemo vitabuni. Nikiendelea namna hii, nitachapisha kitabu kingine, labda kiitwe "Cross Cultural Conversations." Itachukua muda, bila shaka miaka kadhaa.

Friday, May 20, 2022

USHIRIKI WANGU KATIKA MATAMASHA

 

Mimi kama mwandishi, ninashiriki matamasha ya vitabu na tamaduni, kama inavyoonekana pichani. Hii ni fursa kwangu ya kufahamiana na watu, kuwajulisha kuhusu shughuli zangu kama mwalimi na mwandishi, na pia kusikia mawazo na mitazamo yao. Ni fursa pia ya watu kujipatia vitabu vyangu.

Ushiriki wangu kwenye shughuli hizi una manufaa kwangu na kwa jamii. Hayo huelezwa katika vyombo vya habari, na mfano ni huu hapa.

Mimi mwenyewe nimetamka mara kwa mara kuwa nayaona matamasha haya kama darasa, ambamo nafundisha na kujifunza.


Monday, May 16, 2022

VITABU VYANGU, NAFSI YANGU

Vitabu vyangu si vitu vilivyo nje yangu. Ni sehemu ya nafsi yangu, kama kilivyo kichwa changu au ulivyo moyo wangu. Haiwezekani kuvitenganisha na mimi mwenyewe.

Ninaandika vitabu si tu ili watu waifahamu mada, bali pia ili wanifahamu. Kwa hiyo, sielei angani kwa nadharia na hoja zisizofikika kirahisi. Ninaongelea mambo yanayomgusa binadamu. Vitabu hivi ni sauti yangu na pumzi yangu.

Nitakapokuwa siko diniani, vitabu hivi vitaendelea kuongea na walimwengu, vikiwasilisha sauti yangu. Kwa njia ya kazi zao, waandishi tangu kale wametamani na wamefanikiwa kuishi hata baada ya kufariki.

Gilgamesh, shujaa wa kale wa Mesopotamia, alitamani hivyo, akataka kuandika jina lake, lisitoweke. Akina Shakespeare na Shaaban Robert bado tunao, kadhalika akina Tolstoy, Muyaka, Achebe na wengine kwa maelfu.

Wednesday, May 11, 2022

Mpiga Debe Mpya

Nimeanzisha programu ya mazungumzo mtandaoni Zoom ninayoyaita "Cross Cultural Conversations." Nilianza tarehe 16 Aprili, na ninafanya kila Jumamosi, saa kumi na mbili jioni hadi saa moja na nusu kwa saa za Afrika Mashariki.

Siku mojawapo, baada ya mhadhara wangu juu ya "Money in African and American Culture," mhudhuriaji aitwaye Kelly aliweka picha ya vitabu vyangu kwenye ukurasa wake wa Facebook, pamoja na ujumbe huu:

Beautiful afternoon to sit in Miss Samantha's yard! I'm reading work from Joseph Mbele, suggested by my friend Anita. Joseph is leading a recurring Zoom call on Saturday mornings (10 to 11:30) with intriguing conversations, focusing on different topics. My inbox is always open, I'd be happy to share the next Eventbrite link.

Imetokea hivyo, kwamba tangu nianze programu hii, wahudhuriaji wamekuwa wapiga debe wangu wakuu. Wanawaambia wengine na kuwashawishi wahudhurie. Matangazo ya mada ninaweka Facebook siku chache kabla ya mhadhara. Yeyote anakaribishwa kujisajili kwa kutumia linki inayoambatishwa kwenye tangazo.

Tangazo la Maongezi Yangu Books on Central, Faribault

Kwa miaka mingi, nimeongea na hadhira mbali mbali hasa kuhusu tofauti za tamaduni. Matangazo huandaliwa na kusambazwaa kabla ya mikutano. Ka...