Friday, May 20, 2022

USHIRIKI WANGU KATIKA MATAMASHA

 

Mimi kama mwandishi, ninashiriki matamasha ya vitabu na tamaduni, kama inavyoonekana pichani. Hii ni fursa kwangu ya kufahamiana na watu, kuwajulisha kuhusu shughuli zangu kama mwalimi na mwandishi, na pia kusikia mawazo na mitazamo yao. Ni fursa pia ya watu kujipatia vitabu vyangu.

Ushiriki wangu kwenye shughuli hizi una manufaa kwangu na kwa jamii. Hayo huelezwa katika vyombo vya habari, na mfano ni huu hapa.

Mimi mwenyewe nimetamka mara kwa mara kuwa nayaona matamasha haya kama darasa, ambamo nafundisha na kujifunza.


No comments:

Tangazo la Maongezi Yangu Books on Central, Faribault

Kwa miaka mingi, nimeongea na hadhira mbali mbali hasa kuhusu tofauti za tamaduni. Matangazo huandaliwa na kusambazwaa kabla ya mikutano. Ka...