Wednesday, May 11, 2022

Mpiga Debe Mpya

Nimeanzisha programu ya mazungumzo mtandaoni Zoom ninayoyaita "Cross Cultural Conversations." Nilianza tarehe 16 Aprili, na ninafanya kila Jumamosi, saa kumi na mbili jioni hadi saa moja na nusu kwa saa za Afrika Mashariki.

Siku mojawapo, baada ya mhadhara wangu juu ya "Money in African and American Culture," mhudhuriaji aitwaye Kelly aliweka picha ya vitabu vyangu kwenye ukurasa wake wa Facebook, pamoja na ujumbe huu:

Beautiful afternoon to sit in Miss Samantha's yard! I'm reading work from Joseph Mbele, suggested by my friend Anita. Joseph is leading a recurring Zoom call on Saturday mornings (10 to 11:30) with intriguing conversations, focusing on different topics. My inbox is always open, I'd be happy to share the next Eventbrite link.

Imetokea hivyo, kwamba tangu nianze programu hii, wahudhuriaji wamekuwa wapiga debe wangu wakuu. Wanawaambia wengine na kuwashawishi wahudhurie. Matangazo ya mada ninaweka Facebook siku chache kabla ya mhadhara. Yeyote anakaribishwa kujisajili kwa kutumia linki inayoambatishwa kwenye tangazo.

No comments:

Tangazo la Maongezi Yangu Books on Central, Faribault

Kwa miaka mingi, nimeongea na hadhira mbali mbali hasa kuhusu tofauti za tamaduni. Matangazo huandaliwa na kusambazwaa kabla ya mikutano. Ka...