Saturday, May 27, 2023

Kijitabu Hiki Kiuzwe Angalau Shilingi Milioni Moja

WaTanzania wenzangu, nimechapisha kijitabu, "Notes on 'Song of Lawino'" na sasa naleta hoja kuhusu bei yake.
Kijitabu hiki nimekiandika kutokana na jinsi ninavyoipenda fasihi. Nilipenda kuandika uchambuzi wa "Song of Lawino." Nimetumia miaka mingi kutafakari na kuandika. Ingekuwa ninalipwa kwa kila saa na siku niliyofanya hiyo kazi, ningekuwa tajiri.
Kwa maneno mengine, ingekuwa masaa yale yote na siku zile zote nimetumia kutengeneza na kuuza mkaa au kwenye ajira katika ofisi fulani, ukizingatia elimu yangu, ningekuwa nimeingiza mfukoni mamilioni ya shilingi.
Sasa kumbe matokeo ya shughuli yote hii ni kijitabu cha kurasa 70 tu. Watu watauliza bei yake ni shilingi ngapi. Ni dola 12, ambayo ni karibu shilingi 28,000. Najua kuwa wako watakaoshangaa bei hiyo kwa kijitabu cha kurasa chache.
Je, bei ya kitabu inawakilisha nini? Ndio thamani ya kitabu? Yaani tafakari yote na mawazo yote yaliyomo humu thamani yake ni hii shilingi 28,000? MTanzania akienda baa na hizi hela, atakunywa bia ngapi? Je kitabu hiki thamani yake ni sawa na hizi bia chache?
Binafsi, nakataa. Inatakiwa kitabu hiki kiuzwe angalau shilingi milioni moja. Angalau milioni moja, ukizingatia jasho nililotoa, na mikwamo niliyopitia. Niliyoandika humu nayaona kuwa ya thamani kubwa. Angalau kiuzwe milioni moja. Shilingi 28,000 ni dhuluma tupu, mchana kweupe.
Halafu, hiki ni kitabu ambacho hakitanunuliwa, labda na watu wachache sana. Huenda zisiuzwe nakala 10. Kingekuwa kitabu cha udaku, kingeuzika kwa kiasi fulani. Lakini hiki ni kitabu kikavu cha kitaaluma. Kitasota bila wateja. Hakitaniletea hela, labda visenti vichache. Ni kazi isiyo na ujira.
Mimi siandiki vitabu kwa ajili ya kupata hela. Nilitumia muda wangu wote huu kuandika hiki kitabu nikijua kuwa hakitauzika, labda nakala chache sana. Kinachonifanya niandike si pesa bali kuipenda kwangu fasihi. Nitaendelea kuandika.

 

Sunday, February 26, 2023

Mdau Kajipatia Vitabu

Jana ndugu aitwaye John Oketch kaweka picha katika ukurasa wa Facebook uitwao Africans in the United States, akiwa ameshika kitabu changu Chickens in the Bus: More Thoughts on Cultural Differences. Ameambatanisha ujumbe akiwahimiza watu wajipatie nakala ya kitabu hiki. Picha hii imenivutia sana. Naona imepigwa kwa ustadi mkubwa.

>

Baadaye, ndugu Oketch aliweka hii picha nyingine, na ujumbe huu: thank you professor. I am grateful for your writing especially for my 4 kids who are born and raised in America. I have added your books to our African collection. Would you be kind to please share the link again in the reply just incase someone would like a copy.

Tafsiri: asante profesa. Nashukuru kwa uandishi wako hasa kwa ajili ya watoto wangu wanne ambao wamezaliwa na kulelewa hapa Marekani. Nimeviweka vitabu vyako katika maktaba yetu ya vitabu kuhusu Afrika. Je, unaweza, tafadhali, kuweka tena linki ya vitabu endapo kuna atakayehitaji nakala?

Nami nimeweka linki hii kwenye ukurasa ule wa Facebook.

Saturday, December 17, 2022

Cross Cultural Conversation With an American Student

Sophia ni mwanafunzi wangu hapa katika Chuo cha St. Olaf. Ni mfuatiliaji wa maandishi na maongezi yangu YouTube kuhusu tofauti za tamaduni. Siku chache zilizopita, aliniambia kuwa amepata kitabu changu, Chickens in the Bus: More Thoughts on Cultural Differences. Aliniambia kuwa angependa tufanye mahojiano. Leo, tarehe 17 Desemba, tumekutana ofisini mwangu tukaongelea mengi.

Kijitabu Hiki Kiuzwe Angalau Shilingi Milioni Moja

WaTanzania wenzangu, nimechapisha kijitabu, "Notes on 'Song of Lawino'" na sasa naleta hoja kuhusu bei yake. Kijitabu hiki...