Hapa Kwetu
Saturday, December 17, 2022
Cross Cultural Conversation With an American Student
Sunday, November 27, 2022
Monday, October 24, 2022
Mdau Amechapisha Mapitio ya Kitabu Changu
Saturday, October 1, 2022
Nimekutana na Wasomaji Wangu
.jpg)
Sarah na mimi tumefahamiana tangu Julai 2019, aliponikuta kwenye maonesho ya vitabu mjini Blaine, Minnesota, akaipatia kitabu cha "Africans and Americans: Embracing Cultural Differences."
Baadaye Sarah alichapisha kitabu cha mashairi yake kiitwacho "Vita, Babel, Cauliflower," ambacho nilikisoma nikakifurahia, na kisha nikakiandikia uhakiki. Unaweza kuona kisehemu cha uhakiki wangu kwenye tovuti ya Amazon. Sarah ana kipaji kikubwa cha utunzi wa mashairi ya kiIngereza.
Katika maongezi yetu ya leo, nimefahamu kuwa baada ya kusoma kitabu changu cha "Africans and Americans: Embracing Cultural Differences," Sarah alianza kumwelezea rafiki yake wa miaka mingi Brighid juu yangu na kitabu hiki..
Kutokana na hayo, Brighid alifurahi sana kukutana nami leo. Alikuwa na nakala ya kitabu, kikiwa kimepigiwa mistari kwenye vifungu na sentensi nyingi, kuashiria kuwa amekuwa akisoma kwa uangalifu na tafakuri tele. Nilishangaa anavyokumbuka hata mambo madogo yaliyomo kitabuni.
Tuliongea kwa masaa matatu, na muda mwingi tuliongelea tofauti za tanmadunni nilizozielezea kitabuni. Lakini pia tuliongelea uwezekano wa kushirikiana katika utatuzi wa mahitaji mbali mbali katika jamii za Afrika Mashariki, kama vile elimu na maji. Tumefurahi kugundua kuwa wote tayari tumekuwa tukifanya hayo. Brighid, kwa mfano amekuwa akifanya shughuli hizi Arusha. Tumehamasika kufanya zaidi.
Sunday, September 25, 2022
Mkutano na Mmiliki wa African Travel Seminars
Zaidi ya hayo, Georgina ni kati ya wale wanaotumia kitabu changu cha Africans and Americans: Embracing Cultural Differences katika shughuli zao. Kuafiki kwao yale ninayosema kuhusu utamaduni wa waAfrika kunsnifanya nijisikie vizuri. Hiyo juzi nilimkabidhi kitabu changu kipya, Chickens in the Bus: More Thoughts on Cultural Differences.
Sunday, September 18, 2022
Tanga Watafakari Changamoto za Tofauti za Tamaduni


Mratibu wa kikundi, Georgina, alikuwa amesoma kitabu changu, Africans and Americans: Embracing Cultural Differences, wakati niko bado Marekani, akaamua kunialika kuongea nao.
Safari yangu kutoka Marekani nilitua Nairobi, nikapitiliza hadi Mombasa. Kutokea Mombasa, nilishuka Tanga. Nilipumzika siku moja nikisubiri mkutano. Mkutano tulifanyia Hashtag Cafe, na ulifana sana. Wadau walifurahia kunisikiliza, tukabadilishana uzoefu na mitazamo. Nilikuwa nimeleta nakala za vitabu vyangu: Matengo Folktales, Africans and Americans: Embracing Cultural Differences, na Chickens in the Bus: More Thoughts on Cultural Differences. Wadau walivinunua.
Kuanzishwa kwa Cross Cultural Dialogue ni jambo muhimu sana. Dunia inavyozidi kuwa kijiji, watu wa tamaduni mbali mbali, tupende tusipende, tunajikuta katika mahusiano ya kila aina ambayo huja na changamoto nyingi, ndogo na kubwa, kwa sababu ya tofauti za tamaduni. Tofauti hizi zinaweza kukwamisha au kuharibu mahusiano, iwe ni ya binafsi, biashara, diplomasia, na kadhalika.
Sunday, May 22, 2022
Huenda Nikaandika Kitabu Kingine Kuhusu Tamaduni
Tarehe 25 Agosti, 2021, nilichapisha kitabu, Chickens in the Bus: More Thoughts on Cultural Differe=-ians and Americans: Embracing Cultural Differences." Baada ya kuchapisha vitabu hivi, niliona sina haja ya kuandika kitabu kingine juu ya tamaduni.
Cross Cultural Conversation With an American Student
Sophia ni mwanafunzi wangu hapa katika Chuo cha St. Olaf . Ni mfuatiliaji wa maandishi na maongezi yangu YouTube kuhusu tofauti za tamaduni....

-
Leo ni kumbukumbu ya siku ya kuzaliwa kwangu, ambayo ni tarehe 17 Agosti, 1951. Familia yangu, ndugu, na marafiki wamejumuika nami kushereh...
-
Leo napenda kukitambulisha kwako mdau kitabu muhimu cha ki-Swahili, Tenzi Tatu za Kale . Nilinunua nakala yangu miaka kadhaa iliyopita katik...
-
Kutafsiri kazi ya fasihi ni kazi ngumu ya kuchemsha bongo. Inahitaji ufahamu wa hali ya juu wa lugha husika, na pia hisia makini za kifasih...