Saturday, February 10, 2024

Taarifa fupi ya Mhadhara Mjini Owatonna.

Tarehe 8 Februari, nilikwenda mjini Owatonna, hapa katika jimbo la Minnesota. Nilikuwa nimelikwa na mkurugenzi wa Owatonna Public Library kutoa mhadhara juu ya changamoto za tofauti za tamaduni baina ya waAfrika na waMarekani.

Mahudhurio yalikuwa makubwa, kwa mujibu wa mkurugenzi. Miongoni mwa wahudhuriaji alikuwa bwana Tim Penny ambaye aliwa kuwa mjumbe katika bunge la wawakilishi hapa nchini Marekani.

Mhadhara ulikwenda vizuri, na wahudhuriaji walikuwa na masuali ya kusisimua. Kikao kilipoisha, watu walinunua vitabu, na mmoja wao alikuwa bwana Tim Penny aonekanaye pichani. Aliwahi kuwa mjumbe katika Baraza la Wawakilishi la Marekani.

No comments:

Tangazo la Maongezi Yangu Books on Central, Faribault

Kwa miaka mingi, nimeongea na hadhira mbali mbali hasa kuhusu tofauti za tamaduni. Matangazo huandaliwa na kusambazwaa kabla ya mikutano. Ka...