Sunday, January 14, 2024

Vitabu Vinaenda Iran

 Tarehe 12 Januari, 2024, nilisafirisha vitabu vyangu viwili, Africans and Americans: Embracing Cultural Differences na Chickens in the Bus: More Thoughts on Cultural Differences, kwenda Tehran, Iran, kwa mwendesha kipindi cha televisheni kiitwacho THE ENLIGHTENMENT SHOW. Hii ilikuwa ni baada ya yeye kufanya mahojiano nami, akiwa amelenga zaidi kwenye mada ya fasihi ya Afrika na ukoloni, na pia mitazamo ya waMarekani kuhusu Afrika.

Mahojiano tulifanya kwa Zoom, na hii ilikuwa mara yangu ya kwanza kufanyiwa mahojiano Iran. Ninasubiri kwa hamu kupata mrejesho kutoka kwa watu wa kule, hasa baada ya vitabu vyangu kuwafikia.


No comments:

Tangazo la Maongezi Yangu Books on Central, Faribault

Kwa miaka mingi, nimeongea na hadhira mbali mbali hasa kuhusu tofauti za tamaduni. Matangazo huandaliwa na kusambazwaa kabla ya mikutano. Ka...