Saturday, December 25, 2021

Krismasi Katika Fasihi

Pamoja na mambo mengine, fasihi inaweza kubeba tafakari au taswira ya yale tunayokutana nayo maishani.Leo, siku ya Krismasi, napenda kuanzisha tafakari juu ya fasihi na Krismasi. Kwa upande wangu, kazi za fasihi ninazozikumbuka wakati huu wa Krismasi ni hizi:

1) "A Christmas Carol" (hadithi ya Charles Dickens)
2) "Journey of the Magi" (shairi la T.S. Eliot)
3) "Christ Climbed Down" (shairi la Lawrence Ferlinghetti)

Kazi hizi zote zina mambo mengi yanayohusu Krismasi na pia yanayogusa hisia kwa umahiri wa sanaa. KiIngereza kilivyotumika katika "Journey of the Magi," kwa mfano, kinagusa sana, na ubunifu wa simulizi yake ni wa kusisimua. Ninajiona mwenye bahati kuifahamu lugha hiyo vizuri sana, kwa undani kabisa, na ninafaidi uhondo.

Kwa upande mwingine, shairi la Ferlinghetti linasisimua kwa jinsi linavyokejeli kugeuzwa kwa Krismas kuwa si tukio la kidini bali la kibiashara. Kwa maana hiyo, Ferlinghetti anatukumbusha yale waliyoandika akina Marx na Engels katika "Communist Manifesto" kuhusu namna ubepari unavyohujumu na kunajisi mambo mbali mbali.

Huu ni wakati wa muafaka kwa wapenzi wa fasihi kutafuta tungo hizi, na zingine, kuzisoma au kurudia kuzisoma, na kuzitafakari.

Tangazo la Maongezi Yangu Books on Central, Faribault

Kwa miaka mingi, nimeongea na hadhira mbali mbali hasa kuhusu tofauti za tamaduni. Matangazo huandaliwa na kusambazwaa kabla ya mikutano. Ka...