Thursday, August 5, 2021

Msomaji Wangu Amefariki


Leo, tarehe 5 Agosti, niliamua kuanglia ujumbe niliochapisha kwenye blogu yangu mojawapo uitwao "Book Reviewed in 'The Zumbro Current.'" Ujumbe uliambatana na tahakiki ya kitabu changu, Africans and Americans: Embracing Cultural Differences. Niliamua kufuatilia taarifa za mhakiki, Duane Charles Hoven, nikagundua kuwa alifariki miezi iliyopita, na hapa ni taarifa ya kufariki kwake.

Nimesikitika, hasa kwa kuwa sikuwahi kumwona, ingawa maskani yake ni maili thelathini tu kutoka hapa nilipo. Uhusiano wetu ni zaidi ya huu wa mwandishi na msomaji wake. Mchungaji Duane alisomea katika chuo cha St. Olaf ambapo ninafundisha, na alikuwa mjumbe wa bodi ya wakurugenzi wa chuo. Apumzike kwa amani.

Uhakiki wake wa kitabu changu ni huu hapa:

Book Review: Africans and Americans: Embracing Cultural Differences

The Abner Haugen Library at Zumbro Lutheran Church has a copy of this extremely helpful book on cultural differences between Americans and Africans. It is written by Joseph L. Mbele, a Tanzanian scholar who currently is a professor of English at St. Olaf College. Anyone traveling to another country or continent would find this short book well worth reading. A few of the topics covered are: eye contact, personal space, gender issues, gifts, how “time flies, but not in Africa.” Both my wife Ann and I recommend this 98-page book.

-Duane Charles Hoven. "The Zumbro Current," October 2014, p. 7.

Tangazo la Maongezi Yangu Books on Central, Faribault

Kwa miaka mingi, nimeongea na hadhira mbali mbali hasa kuhusu tofauti za tamaduni. Matangazo huandaliwa na kusambazwaa kabla ya mikutano. Ka...