Ujumbe kwa Rais Magufuli: Shirikiana na UKAWA

Mheshimiwa Rais Magufuli, salaam na pole kwa majukumu ya kutumbua majipu. Mimi ni raia wako, ambaye si mwanachama wa chama chochote cha siasa. Nimeona nikuandikie, ingawa ninajua kuwa jadi ya ovyo iliyojengwa na chama chako cha CCM ni ya kutotambua uwepo wa sisi raia tusio na vyama. CCM imekuwa na historia ya kutotambua kuwa sisi tusio na chama ni raia wenye haki sawa katika nchi yetu, na wenye akili na mitazamo kuhusu mustakabali wa nchi yetu. Achana na hii jadi. Itakuponza. Ninaandika ujumbe huu kukushauri ushirikiane na UKAWA. Nina sababu za kukushauri hivyo. Kwanza, kumbuka kwamba tangu ulipoingia madarakani kama rais, UKAWA walionyesha mapenzi yao kwako kwa dhati, wakadiriki kutangaza mara kwa mara kwamba ulikuwa unatekeleza ajenda yao. Mheshimiwa Rais Magufuli, hakuna hazina kubwa kwa kiongozi kama kukubalika kiasi hiki. Na katika nchi yenye wapinzani, kuweza kuwakonga nyoyo zao kama ulivyofanya ni jambo la pekee. Ni baraka uliyojaliwa. Tafadhali usiifuje. Sisemi ujiunge na