Sunday, January 14, 2024

Vitabu Vinaenda Iran

 Tarehe 12 Januari, 2024, nilisafirisha vitabu vyangu viwili, Africans and Americans: Embracing Cultural Differences na Chickens in the Bus: More Thoughts on Cultural Differences, kwenda Tehran, Iran, kwa mwendesha kipindi cha televisheni kiitwacho THE ENLIGHTENMENT SHOW. Hii ilikuwa ni baada ya yeye kufanya mahojiano nami, akiwa amelenga zaidi kwenye mada ya fasihi ya Afrika na ukoloni, na pia mitazamo ya waMarekani kuhusu Afrika.

Mahojiano tulifanya kwa Zoom, na hii ilikuwa mara yangu ya kwanza kufanyiwa mahojiano Iran. Ninasubiri kwa hamu kupata mrejesho kutoka kwa watu wa kule, hasa baada ya vitabu vyangu kuwafikia.


Sunday, January 7, 2024

NIMEKABIDHI “CHICKENS IN THE BUS”

Januari 4, 2024, nilikwenda Maple Grove, kukabidhi nakala 20 za Chickens in the Bus: More Thoughts on Cultural Differences kwa mama wa Cameroon ambaye alikuwa ameziagiza kwa ajili ya shule fulani nchini Cameroon.

Katika maongezi, mama huyu alinieleza habari za shule yenyewe, ambayo iko kaskazini magharibi mwa Cameroon, uliko mji wa Bamenda. Alinieleza kwamba lengo lake ni kuwa hivi vitabu visomwe na wanafunzi wa darasa la sita kwenda juu. 

Tuliongelea umuhimu wa kuwafundisha watoto wa kiAfrika juu ya utamaduni wetu, na kuwajenga katika kuuheshimu. Huyu mama alisisitiza kuwa yaliyomo katika Chickens in the Bus yanakidhi malengo hayo.

Mimi kama mwandishi nafurahi sana kujua kuwa watoto wa kiAfrika watakuwa wanasoma na kutafakari kitabu changu 
 

Tangazo la Maongezi Yangu Books on Central, Faribault

Kwa miaka mingi, nimeongea na hadhira mbali mbali hasa kuhusu tofauti za tamaduni. Matangazo huandaliwa na kusambazwaa kabla ya mikutano. Ka...