Juzi, tarehe 5, niliandika katika blogu hii kwamba nilikuwa nimepata barua ya shukrani kutoka Global Minnesota, kufuatia mhadhara niliotoa. Leo, bila kutegemea, nimepata cheki kutoka kwao, kama kifuta jasho.
Sikutegemea, kwani tangu mwanzo waliponialika kutoa mhadhara na hata baada ya mhadhara, sikuwa na hata fununu kwamba kuna kifuta jasho. Nami sikufikiria wala kutegemea. Nilichojali ni kufanya kazi waliyoniomba kufanya, yaani kujadili mada ya "African Folktales to Contemporary Authors."
Ninaongozwa na nasaha ya wahenga kwamba tenda wema nenda zako; usingoje shukrani. Kama nilivyosema katika blogu hii, mengine ni matokeo. Sijawahi kukataa mwaliko wa kwenda kutoa mhadhara kwa sababu ya malipo.
Watu wanaonihimiza nisitoe huduma bila malipo ninawaambia kuwa kuna baraka katika kuwasaidia watu. Fursa ya kutoa mhadhara ni ya manufaa kwangu, kwani inaniongezea uzoefu na kuniwezesha kujitathmini ufahamu wangu, hasa katika kipindi cha masuali na majibu. Vile vile matangazo ya mhadhara yanayoandaliwa na kusambazwa na wale wanaonialika yananiongezea kufahamika.
Mara nyingi, huwezi kujua watu unaowahutubia ni akina nani katika jamii. Nimeshuhudia baada ya mhadhara watu wakijitokeza na kujitambulisha kwangu na kuniuliza iwapo nitakuwa tayari kuhutubia kwenye taasisi au jumuia zao. Mwaliko moja unazaa mialiko mingine. Ninasema hayo ili kuwashawishi wale wanaosita kutoa huduma bila kuahidiwa malipo. Hakuna hasara, bali ni faida.
Sikutegemea, kwani tangu mwanzo waliponialika kutoa mhadhara na hata baada ya mhadhara, sikuwa na hata fununu kwamba kuna kifuta jasho. Nami sikufikiria wala kutegemea. Nilichojali ni kufanya kazi waliyoniomba kufanya, yaani kujadili mada ya "African Folktales to Contemporary Authors."
Ninaongozwa na nasaha ya wahenga kwamba tenda wema nenda zako; usingoje shukrani. Kama nilivyosema katika blogu hii, mengine ni matokeo. Sijawahi kukataa mwaliko wa kwenda kutoa mhadhara kwa sababu ya malipo.
Watu wanaonihimiza nisitoe huduma bila malipo ninawaambia kuwa kuna baraka katika kuwasaidia watu. Fursa ya kutoa mhadhara ni ya manufaa kwangu, kwani inaniongezea uzoefu na kuniwezesha kujitathmini ufahamu wangu, hasa katika kipindi cha masuali na majibu. Vile vile matangazo ya mhadhara yanayoandaliwa na kusambazwa na wale wanaonialika yananiongezea kufahamika.
Mara nyingi, huwezi kujua watu unaowahutubia ni akina nani katika jamii. Nimeshuhudia baada ya mhadhara watu wakijitokeza na kujitambulisha kwangu na kuniuliza iwapo nitakuwa tayari kuhutubia kwenye taasisi au jumuia zao. Mwaliko moja unazaa mialiko mingine. Ninasema hayo ili kuwashawishi wale wanaosita kutoa huduma bila kuahidiwa malipo. Hakuna hasara, bali ni faida.