Wednesday, February 9, 2022

Vitabu Viko Chuoni Mbeya

 

Tarehe 27 hadi 29 Januari, 2022, nilikuwa mgeni wa Catholic University College of Mbeya. Nilikuwa nimealikwa kutoa mhadhara juu ya “Africans and Americans: Embracing Cultural Differences.” Lakini nilijikuta katika shughuli zingine pia, ikiwemo mazungumzo na waalimu na pia mkuu wa chu

 

Katika mhadhara wangu, niliibua masuala ambayo nimeyaongelea katika vitabu vyangu Africans and Americans: Embracing Cultural Differences na Chickens in the Bus: More Thoughts on Cultural Differences. Lengo langu kuu lilikuwa kuanzisha jadi ya kutafakari changamoto za tofauti za tamaduni katika ulimwengu wa utandawazi wa leo.

Tafakari hii inapaswa iwe endelevu. Kuchangia hilo, nilikabidhi nakala za hivi vitabu vyangu viwili kwa ajili ya maktaba ya chuo. Baadaye mkurugenzi  wa maktaba ameniandikia ujumbe wa shukrani kwa kupewa vitabu hivyo. 

No comments:

Tangazo la Maongezi Yangu Books on Central, Faribault

Kwa miaka mingi, nimeongea na hadhira mbali mbali hasa kuhusu tofauti za tamaduni. Matangazo huandaliwa na kusambazwaa kabla ya mikutano. Ka...