Monday, February 27, 2017

Mahojiano: Beca Lewis na Joseph Mbele

Miezi michache iliyopita, jirani yangu mmoja, mama Mmarekani, aitwaye Merrilyn, ambaye ni mpiga debe wa maandishi na shughuli zangu za uelimishaji, alimwelezea habari zangu rafiki yake aishiye Ohio. Halafu alimpelekea kitabu changu cha Africans and Americans: Embracing Cultural Differences. Wakati huo huo, alituunganisha kupitia mtandao wa Facebook.

Beca Lewis, nilikuja kufahamu, ni mwandishi, mwelimishaji, na mmiliki na mwendeshaji wa kituo cha mawasiliano kiitwacho The Shift. Kutokana na alivyomsikia rafiki yake Merrilyn na kutokana na kusoma kitabu changu, Beca Lewis aliniuliza kama ningekubali kufanya mahojiano naye. Nilivyokubali, tulipanga siku, tukafanya mahojiano tarehe 14 Februari, saa tano asubuhi.

Leo, Beca Lewis ameyaweka mahojiano yetu hewani, nami nayaleta hapa katika blogu yangu:
http://theshift.com/podcast/every-culture-is-weird-and-wonderful/

No comments:

Tangazo la Maongezi Yangu Books on Central, Faribault

Kwa miaka mingi, nimeongea na hadhira mbali mbali hasa kuhusu tofauti za tamaduni. Matangazo huandaliwa na kusambazwaa kabla ya mikutano. Ka...