Wednesday, August 12, 2020

Duka Jipya la Vitabu Vyangu

Vitabu vyangu viwili, Africans and Americans: Embracing Cultural Differences na Matengo Folktales sasa vinapatikana katika duka la taasisi iitwayo Planting People Growing Justice.

Mwanzilishi na mwendeshaji wa taasisi hiyo, Dr. Artika Tyner, ni profesa wa sheria katika Chuo Kikuu cha St. Thomas hapa Minnesota. Aliniuliza iwapo nitaridhia vitabu vyangu kuuzwa na taasisi hiyo.

Alianza kukifahamu kitabu changu mwaka juzi, baada ya kununua nakala kadhaa kwa ajili ya watu aliowapeleka Ghana katika safari ya kielimu akishirikiana na Monica Habia,  mwanazuoni mwenzake kutoka Ghana. Baada ya safari hiyo, Monica alinielezea jinsi kitabu kilivyowasaidia waMarekani kuyaelewa mambo waliyokutana nayo Ghana.

Unaweza kutembelea tovuti ya Planting People Growing Justice. Vitabu hivi viwili vinapatikana Tanzania, katika maduka ya Soma Book Cafe na A Novel Idea.

No comments:

Tangazo la Maongezi Yangu Books on Central, Faribault

Kwa miaka mingi, nimeongea na hadhira mbali mbali hasa kuhusu tofauti za tamaduni. Matangazo huandaliwa na kusambazwaa kabla ya mikutano. Ka...