Friday, May 28, 2021

Nimealikwa Kuongelea Kitabu Changu

Nimealikwa kuongelea kitabu changu, Africans and Americans: Embracing Cultural Differences, katika mkutano mkubwa ujulikanao kama Trade With Africa Summit utakaofanyika kutumia mtandao tarehe 31 Mei hadi 4 Juni mwaka huu. Mkutano huu hufanyika mara moja kwa mwaaka.

Aliniaalika ni mwanaadji waa mkutano Toyin Umesiri, mjasiriamali na mhamasishaji maarufu wa biashara baina ya Afrika na nchi zingine, hasa Marekani. Aliamua kunialika baada ya kusoma kitabu changu kisha akanialika kwenye kipindi chake cha Nazaru TV na kufanya mahojiano nami.

Kwa miezi ya karibuni, mimi mwenyewe nimeanza kujibidisha kutafiti namna tofauti za tamaduni zinavyoathiri biashara. Mawazo yangu tayari yanaonekana katika kitabu changu, lakini ninayaendeleza na kuyafafanua. Mfano ya juhudi zangu ni makala katika Medium na maongezi katika YouTube.

No comments:

Tangazo la Maongezi Yangu Books on Central, Faribault

Kwa miaka mingi, nimeongea na hadhira mbali mbali hasa kuhusu tofauti za tamaduni. Matangazo huandaliwa na kusambazwaa kabla ya mikutano. Ka...