Sunday, September 5, 2021

Msomaji wa Kwanza wa Kitabu Changu Kipya

Jana, tarehe 4 Septemba, 2021, nilipata nakala za kitabu changu kipya Chickens in the Bus: More Thoughts on Cultural Differences. Hima nilimpa nakala jirani yangu, Mama Merri, mwalimu mstaafu anayependa sana kusoma maandishi yangu na ni mfuatiliaji wa shughuli zangu za kuelimisha waMarekani kuhusu utamaduni wa Afrika na tofauti zake na ule wa Marekani. 

Ni bahati njema kwa mwandishi kuwa na wasomaji na wafuatiliaji wa aina ya huyu mama. Lakini kwa hapa Marekani, bahati hiyo ninayo sana. Nina wasomaji na wafuatiliaji wengi.

Mama Merri alifundisha kwa miaka mingi katika shule za waHindi Wekundu. Alivyosoma kitabu changu Africans and Americans: Embracing Cultural Differences aliandika maelezo kuhusu namna utamaduni wao unavyofanana na ule wa waAfrika nilioelezea kitabu. Ninashukuru kwa elimu anayonipa.


 

No comments:

Tangazo la Maongezi Yangu Books on Central, Faribault

Kwa miaka mingi, nimeongea na hadhira mbali mbali hasa kuhusu tofauti za tamaduni. Matangazo huandaliwa na kusambazwaa kabla ya mikutano. Ka...