Tuesday, March 6, 2018

Mdau wa Kitabu Amekuja Tena

Hapa pichani ninaonekana na De'Vonna, mmoja wa waandaaji wa maonesho ya waandishi yaliyoitwa Minnesota Black Authors Expo, ambayo niliyaelezea katika blogu hii. Anaonekana ameshika kitabu changu, Africans and American:Embracing Cultural Differences. Picha tulipiga wakati wa maonesho. Amenilitea ujumbe kuwa anahitaji nakala nyingine ya hiki kitabu.

Kwa kuzingatia jinsi mama huyu alivyo na ushawishi katika jimbo hili la Minnesota, hasa miongoni mwa wenzake wa-Marekani Weusi, nimeguswa na ujumbe wake kwa namna ya pekee. Tangu nilipoandika kitabu hiki, nilikuwa na dukuduku ya kujua wa-Marekani Weusi watakuwa na maoni gani kuhusu yale ninayosema juu ya mahusiano yao na sisi wa-Afrika. Nilielezea dukuduku hiyo katika blogu ya ki-Ingereza.

Kama inavyoeleweka, mahusiano hayo yanawatatiza baadhi ya watu. Kwa hivyo ninapopata mrejesho kutoka kwa hao wenzetu, ninauchukulia kwa uzito wa pekee. Nimefarijika na kufurahi kwamba De'Vonna anataka nakala nyingine ya kitabu changu. Sijui anakipeleka wapi, au atakitumia vipi, lakini hii si hoja.

No comments:

Tangazo la Maongezi Yangu Books on Central, Faribault

Kwa miaka mingi, nimeongea na hadhira mbali mbali hasa kuhusu tofauti za tamaduni. Matangazo huandaliwa na kusambazwaa kabla ya mikutano. Ka...