Thursday, December 5, 2019

Maongezi Kuhusu Fasihi Simulizi ya Africa

Jana jioni, kwa mwaliko wa chama cha wanafunzi kiitwacho Karibu, nilitoa mhadhara hapa chuoni St. Olaf kuhusu fasihi simulizi ya Afrika. Tuna wanafunzi wachache kutoka Afrika, lakini wanajitahidi kuitangaza Afrika kwa namna mbali mbali, kama vile mihadhara, filamu, ngoma, muziki, michezo ya kuigiza, na maonesho ya mavazi.

Mara kwa mara wananialika kuelezea utamaduni wa Afrika, hasa unavyojitokeza katika fasihi simulizi. Nami hupenda kufanya hivyo. Ninauenzi mchango wa Afrika duniani. Afrika ni chimbuko la binadamu. Ni chimbuko la tekinolojia, sayansi, lugha, fasihi, falsafa, na kadhalika.

Hiyo jana nilelezea hayo, nikaleta methali kadhaa kuthibitisha uzito wa falsafa ya wahenga wetu kuhusu masuala ya maisha na maadili. Tulitafakari methali hizo, na mwishoni nilisimulia hadithi iitwayo "The Donkey Who Sinned," iliyomo katika kitabu cha Harold C. Courlander kiitwacho A Treasury of African Folklore. Nayo tuliitafakari, kwa jinsi inavyoonyesha athari za ubabe kwa wale wasio na nguvu. Katika hadithi hiyo, wenye mabavu wanaogopwa hata pale wanapokosea, na asiye na nguvu anadhulumiwa.

No comments:

Tangazo la Maongezi Yangu Books on Central, Faribault

Kwa miaka mingi, nimeongea na hadhira mbali mbali hasa kuhusu tofauti za tamaduni. Matangazo huandaliwa na kusambazwaa kabla ya mikutano. Ka...