Monday, February 24, 2020

Sherehe ya African Travel Seminars

Juzi tarehe 22, Ilifanyika sherehe mjini Minneapolis ya kutimiza miaka 24 ya kampuni ya African Travel Seminars. Niliwahi kuandika taarifa katika blogu hii. Waalikwa walikuwa watu waliowahi kusafiri na kampuni hii ya utalii ambayo hupeleka watu kwenye nchi kama vile Ghana, Senegal, Gambia, Morocco, Misri, Ethiopia, Kenya, Tanzania, Afrika Kusini, Cuba na na Brazil. Walialikwa pia marafiki wa kampuni.  Nilipata fursa ya kusema machache, nikaongelea utalii kama nyenzo ya elimu na ujenzi wa mahusiano baina ya mataifa na tamaduni.

Mmiliki na mkurugenzi wa African Travel Seminars, Georgina Lorencz, aliniagiza nipeleke nakala za kitabu changu, Africans and Americans: Embracing Cultural Differences, ambacho siku za karibuni ameanza kukipendekeza kwa wadau naowapeleka Afrika. Nilipeleka pia nakala za Matengo Folktales kuwa kuwa nilijua kuwa katika hotuba yangu ningetaja umuhimu wa kuelewa misingi ya utamaduni na falsafa ya wahenga wetu wa Afrika.


Kulikuwa pia na vyakula vha kiAfrika. Baadhi ya mambo yaliyofanyika katika sherehe ni zoezi la kujibu maswali mbali mbali kuhusu Afrika. Watu walivutiwa na zoezi hili lililokuwa ni chemsha bongo. Baadhi ya masuali ninayoyakumbuka ni haya: kiSwahili ni lugha ya taifa ya chi zipi? Nchi ipi imetoa washindi wengi zaidi wa tuzoya Nobel? Mama yupi pekee duniani amewahi kuwa "First Lady" wa nchi mbili?



Washindi walipewa zawadi, zikiwemo nakala za kutabu cha Africans and Americans: Embracing Cultural Differences. Georgina alikuwa ameagiza kuwa kilt mtu agenda akita ameba vazi la kiAfrika. Nami nilijiandaa kwa kununua shati siku mbili kabla ya tukio, kwa sababu mashati yangu mengine nimeshayavaa mara kwa mara miaka iliyopita.
















Palifanyika mashindano ya mavazi kwa lengo la kumtambua mtu aliyetia fora kwa vazi la kiume na hivyo hivyo kwa vazi la kike. Nilipata fursa ya kuongea na watu kadhaa, nikajionea wnavyipenda kampuni ya African Travel Seminars.






Niliona pia watu walivyovutiwa na yale niliyosema, kwa jinsi walivyochangamkia vitabu vyangu na kuvinunua. Mwishoni mwa sherehe, Georgina alitabgaza mipango ya safari zijazo mwaka huu mwezi Septemba na mwakani kwenda Afrika Kusini na Brazil.

No comments:

Tangazo la Maongezi Yangu Books on Central, Faribault

Kwa miaka mingi, nimeongea na hadhira mbali mbali hasa kuhusu tofauti za tamaduni. Matangazo huandaliwa na kusambazwaa kabla ya mikutano. Ka...