Friday, May 1, 2020

Mhadhara Wangu wa Kwanza Kwa Zoom

Tarehe 28 mwezi huu, nilitoa mhadhara kwa wanachuo wa chuoni St. Olaf na wasikilizaji walikuwa Mankato. Mada ilikuwa Understanding Each Other: Brothers and Sisters From Two Continents.

Nimeshahutubia wanachuo wa South Central College mara kadhaa, na ninafurahi kuwa wanaendelea kuwa na hamu ya kunisikiliza, kama inavyoelezwa hapa. Kivutio kimojawapo ni kitabu changu

Hii tarehe 28 ilikuwa ni mara yangu ya kwanza kuhutubia kwa kutumia Zoom. Changamoto ya kuhutubia bila kuiona hadhira kiuhalisia haikosi kuathiri mhadhara. Lakini ripoti nilizopata kutoka kwa mratibu wa mhadhara ni kwamba watt waliufurahia mhadhara wangu, ambao ni huu hapa.

1 comment:

Ndugu Nkwazi N Mhango said...

Siku hizi zoom ni kila kitu inapokuja kwenye mawasiliano. Hata sisi chuo kikuu cha Manitoba tunaitumia sana. Kama usemavyo, changamoto ya kuhutubia ukumbi wa kufikirika ni kubwa. Ila kwa mikutano ni nzuri sana na si haba inasaidia.

Tangazo la Maongezi Yangu Books on Central, Faribault

Kwa miaka mingi, nimeongea na hadhira mbali mbali hasa kuhusu tofauti za tamaduni. Matangazo huandaliwa na kusambazwaa kabla ya mikutano. Ka...