Thursday, June 10, 2021

Nina Wasomaji Butiama kwa Mwalimu Nyerere

Sijawahi kufika Mwitongo, Butiama, lakini kitabu changu, ambacho ni kama nafsi yangu, kimefika. Pichani anaonekana mjukuu wa Mwalimu Nyerere akiwa anasoma kitabu hiki. Picha hii aliiweka mitandaoni akiwa ameambatisha ujumbe. Ninanukuu baadhi ya aliyosema.

"My Dad gave me this book to read this morning, Africans and Americans: Embracing Cultural Differences by Joseph Mbele. I just finished it. One lesson I learned is to respect, understand, and see the value in both cultures. I would highly recommend this book." .................. "My Dad gave me this book, he felt that it could be helpful for me, I’ve lived in the US since I was 7, I’ve made the decision to move back this year. There are many things which I still question. It will be a long learning process, this book has given me hope." .................. "Thank you for writing this book Professor Mbele. I’ve learned quite a lot from reading it but I’ve also grasped a better understanding of many things which haven’t been clear to me before."

Naleta tafsiri yangu kwa kiSwahili:

"Baba alinipa kitabu hiki asubuhi hii nisome, Africans and Americans: Embracing Cultural Differences, cha Joseph Mbele. Nimemaliza sasa hivi. Jambo moja ambalo nimejifunza ni kuheshimu, kuelewa, na kuona thamani ya tamaduni zote mbili. Ninanipendekeza sana kitabu hiki."....

" Baba alinipa kitabu hiki, kwa kuona kwamba kingeweza kunisaidia. Nimeishi Marekani tangu nikiwa na miaka saba, na nimeamua kurejea nyumani mwaka huu. Kuna mambo mengi ambayo bado nayahoji. Itanichukua muda mrefu kujifunza; kitabu hiki kimenipa matumaini."....

"Asante kwa kuandika kitabu hiki Profesa Mbele. Nimmejifunza mengi kwa kukisoma na nimepata uelewa mzuri wa mambo mengi ambayo hayakuwa wazi kwangu."

No comments:

Tangazo la Maongezi Yangu Books on Central, Faribault

Kwa miaka mingi, nimeongea na hadhira mbali mbali hasa kuhusu tofauti za tamaduni. Matangazo huandaliwa na kusambazwaa kabla ya mikutano. Ka...