Tuesday, October 12, 2021

KITABU MUHIMU KWA MAJADILIANO

Tarehe 5 Oktoba, Profesa Artika Tyner anayefundisha sheria katika Chuo Kikuu cha St. Thomas, alikweka picha hii hapa kushoto, akaambatiisha ujumbe huu: "New book alert: This book is an essential guide for intercultural dialogue. Thank you Dr. [Mbele] for sharing knowledge and wisdom." 

Nitafsiri kwa kiSwahili: "Tangazo la kitabu: Kitabu hiki ni mwongozi muhimu kwa majadiliano baina ya tamaduni. Asante Daktari Mbele kwa kutushirikisha ujuzi na hekima."

Profesa Tyner ni mmoja wa maprofesa wanaokitumia kitabu changu cha awali, Africans and Americans: Embracing Cultural Differences, katika masomo. Yeye alianza kukitumia katika programu ya kuwapeleka waMarekani Ghana kujifunza. Ni mmoja wa waMarekani weusi wenye mshikamano na Afrika. Pia ni mwandishi maarufu katika taaluma ya sheria na uongozi, na pia huandika vitabu kwa watoto. 

Kauli yake juu ya kitabu changu ina uzito wa pekee.

No comments:

Tangazo la Maongezi Yangu Books on Central, Faribault

Kwa miaka mingi, nimeongea na hadhira mbali mbali hasa kuhusu tofauti za tamaduni. Matangazo huandaliwa na kusambazwaa kabla ya mikutano. Ka...