Friday, October 15, 2021

Mdau Kajipatia Kitabu

Huyu dada, Tanya, alihudhuria mazungumzo yangu na wana Rotary Club of Brooklyn Park tarehe 6 Oktoba. Mada yangu ilikuwa "Cultural Differences in the Global Village."

Nilipomaliza hotuba yangu, wakati wa masuali na majibu, dada huyu alijitokeza akasema kuwa yeye ni mfanyakazi katika sekta ya elimu na kwamba kwamba alivutiwa na mhadhara wangu akaongeza kuwa mawazo na maudhui yangu yanahitajika mashuleni.

Tulikubaliana kushirikiana kushughulikia changamotto zilizopo mashuleni. Baadaye nilimpelekea hiki kitabu changu, Africans and Americans: Embracing Cultural Differences, kama hatua ya kwanza katika safari yetu hiyo.

No comments:

Tangazo la Maongezi Yangu Books on Central, Faribault

Kwa miaka mingi, nimeongea na hadhira mbali mbali hasa kuhusu tofauti za tamaduni. Matangazo huandaliwa na kusambazwaa kabla ya mikutano. Ka...