Saturday, March 12, 2022

 WADAU WA UTALII KWENYE MHADHARA WANGU ARUSHA

Tarehe 8 Januari, 2022, nilitoa mhadhara Arusha, mada ikiwa "challenges of cultural differences," yaani changamoto za tofauti za tamaduni. Hii ni mada ambayo naiongelea na kuiandikia sana. Mwandaaji wa mhadhara alikuwa mama Ama, mMarekani Mweusi. Walihudhuria watu wa mataifa mbali mbali, lakini zaidi kutoka Marekani na Tanzania. Tuilkaa kwa takriban saa tatu.
Baadhi ya waTanzania waliohudhuria ni vijana wa kampuni ya utalii iitwayo Rift Valley Cultural Tourism, ambayo makao yake ni Karatu. Kupitia kwa mkurugenzi wa kampuni, wote walikuwa wamepata nakala za kitabu changu, Africans and Americans: Embracing Cultural Differences," na walikuwa wamekisoma. 

Waliposikia kuwa ninatoa mhadhara, waliamua kuhudhuria. Tulifurahi kukutana. Baada ya mhadhara, tulipiga hii picha inayoonekana hapa juu; baadhi yao wameshika kitabu changu. Wadau wa utalii ni wanufaika wa moja kwa moja wa kitabu hiki. Hii ilidhihirika mwaka 2007 wakati mkurugenzi wa J.M. Tours aliponunua nakala kadhaa akawapa madreva waongoza watalii wake wasome. 

Walikifurahia kwa msingi kwamba kiliwawezesha katika kushughulika na watalii. Niliandika kuhusu hilo kwenye makala yangu, "My Arusha Readers."
Ninawapongeza Rift Valley Cultural Tourism kwa kutambua fursa na kuitumia. Niko tayari kuwa nao bega kwa bega katika masuala ya utalii na utamaduni, kubadilishana uzoefu na kuelimishana. 

Mbali ya vitabu vyangu, ambavyo vinapatikana mtandaoni, nawakaribisha kwenye chaneli yangu ya YouTube.

No comments:

Tangazo la Maongezi Yangu Books on Central, Faribault

Kwa miaka mingi, nimeongea na hadhira mbali mbali hasa kuhusu tofauti za tamaduni. Matangazo huandaliwa na kusambazwaa kabla ya mikutano. Ka...