Sunday, February 26, 2023

Mdau Kajipatia Vitabu

Jana ndugu aitwaye John Oketch kaweka picha katika ukurasa wa Facebook uitwao Africans in the United States, akiwa ameshika kitabu changu Chickens in the Bus: More Thoughts on Cultural Differences. Ameambatanisha ujumbe akiwahimiza watu wajipatie nakala ya kitabu hiki. Picha hii imenivutia sana. Naona imepigwa kwa ustadi mkubwa.

>

Baadaye, ndugu Oketch aliweka hii picha nyingine, na ujumbe huu: thank you professor. I am grateful for your writing especially for my 4 kids who are born and raised in America. I have added your books to our African collection. Would you be kind to please share the link again in the reply just incase someone would like a copy.

Tafsiri: asante profesa. Nashukuru kwa uandishi wako hasa kwa ajili ya watoto wangu wanne ambao wamezaliwa na kulelewa hapa Marekani. Nimeviweka vitabu vyako katika maktaba yetu ya vitabu kuhusu Afrika. Je, unaweza, tafadhali, kuweka tena linki ya vitabu endapo kuna atakayehitaji nakala?

Nami nimeweka linki hii kwenye ukurasa ule wa Facebook.

No comments:

Kijitabu Hiki Kiuzwe Angalau Shilingi Milioni Moja

WaTanzania wenzangu, nimechapisha kijitabu, "Notes on 'Song of Lawino'" na sasa naleta hoja kuhusu bei yake. Kijitabu hiki...