Friday, April 27, 2012

Nyumbani u-Matengo

Kuna usemi wa ki-Ingereza kwamba uende Mashariki au Magharibi, lakini nyumbani ndio bora zaidi. Tatizo ni kufafanua dhana ya nyumbani. Nikiwa Dar es Salaam, nasema nyumbani ni Songea. Nikiwa Songea nasema nyumbani ni Mbinga. Nikiwa Mbinga nasema nyumbani ni Litembo. Nikiwa huku ughaibuni, naiona Tanzania yote kama nyumbani. Utawasikia wa-Afrika waishio ughaibuni wakisema Afrika ni nyumbani. Dhana ya nyumbani ni tata. Leo napenda kuleta taswira za nyumbani u-Matengo.
Hapa juu ni eneo baina ya Kindimba na Litembo. Zao la ngano linaonekana likiwa tayari kuvunwa.

Hapa kushoto ni sehemu moja karibu na Litembo, kwenye njia itokayo Ngwambo.
Hapa kushoto ni kijijini kwangu Lituru mwendo wa dakika kumi hivi kutoka kwenye nyumba yetu, ukielekea upande wa kushoto. Kule ng'ambo unaonekama mlima maarufu wa Kengema au Likengema, ambao unatazamana na nyumba yetu, kwa ng'ambo.
Hapa kushoto ni misheni Litembo, penye shule na hospitali. Nilizaliwa hapo nikasoma shule ya msingi hapo. Enzi zile, shule ya msingi iliishia darasa la nne. Mlima Kengema unaonekana kule ng'ambo, mrefu kuliko yote. Kwa taarifa zaidi kuhusu Litembo, soma hapa.

1 comment:

Yasinta Ngonyani said...

Ahsante kwa hii...ni kweli mara nyingine mtu unakuwa hujui wapi ni nyumbani...Ila nyumbani ni nyumbani au?...Nimependa jinsi ulivyoandika :-)

Tangazo la Maongezi Yangu Books on Central, Faribault

Kwa miaka mingi, nimeongea na hadhira mbali mbali hasa kuhusu tofauti za tamaduni. Matangazo huandaliwa na kusambazwaa kabla ya mikutano. Ka...