Nimeleta habari hii, ili kukumbushia kuwa maafa hutokea sehemu mbali mbali za dunia, hata katika nchi zenye miundombinu imara na bora kama Marekani. Mbali ya mafuriko, hapa Marekani kuna vimbunga viitwavyo "tornado" ambavyo uharibifu wake hausemeki. "Tornado" ikitua kwenye mji, inavunja majumba na hata kurusha magari hewani na kuyabwaga sehemu tofauti, pengine mbali na pale yalipokuwepo. Sehemu zingine za dunia zinakumbwa na kimbung, sehemu zingine zinakumbwa na tetemeko la nchi na kusababisha uharibifu mkubwa. Hivi karibuni, kwa mfano, tumeshuhudia jinsi sehemu ya mlima ilivyoporomoka kule Afghanistan na kupoteza maisha ya watu wengi na mali zao. Kilichopoo, pamoja na kuchukua tahadhari, kama vile kujenga katika maeneo yanayoonekana yana usalama, tukae tukiomba Mungu atuepushie mbali majanga hayo.
Saturday, June 21, 2014
Mafuriko Marekani
Nimeleta habari hii, ili kukumbushia kuwa maafa hutokea sehemu mbali mbali za dunia, hata katika nchi zenye miundombinu imara na bora kama Marekani. Mbali ya mafuriko, hapa Marekani kuna vimbunga viitwavyo "tornado" ambavyo uharibifu wake hausemeki. "Tornado" ikitua kwenye mji, inavunja majumba na hata kurusha magari hewani na kuyabwaga sehemu tofauti, pengine mbali na pale yalipokuwepo. Sehemu zingine za dunia zinakumbwa na kimbung, sehemu zingine zinakumbwa na tetemeko la nchi na kusababisha uharibifu mkubwa. Hivi karibuni, kwa mfano, tumeshuhudia jinsi sehemu ya mlima ilivyoporomoka kule Afghanistan na kupoteza maisha ya watu wengi na mali zao. Kilichopoo, pamoja na kuchukua tahadhari, kama vile kujenga katika maeneo yanayoonekana yana usalama, tukae tukiomba Mungu atuepushie mbali majanga hayo.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Tangazo la Maongezi Yangu Books on Central, Faribault
Kwa miaka mingi, nimeongea na hadhira mbali mbali hasa kuhusu tofauti za tamaduni. Matangazo huandaliwa na kusambazwaa kabla ya mikutano. Ka...

-
Leo ni kumbukumbu ya siku ya kuzaliwa kwangu, ambayo ni tarehe 17 Agosti, 1951. Familia yangu, ndugu, na marafiki wamejumuika nami kushereh...
-
Leo napenda kukitambulisha kwako mdau kitabu muhimu cha ki-Swahili, Tenzi Tatu za Kale . Nilinunua nakala yangu miaka kadhaa iliyopita katik...
-
Kutafsiri kazi ya fasihi ni kazi ngumu ya kuchemsha bongo. Inahitaji ufahamu wa hali ya juu wa lugha husika, na pia hisia makini za kifasih...
2 comments:
mungu awape subra hao wananchi, ila Tanzania tukubali Kule mabondeni na Kama Gongolamboto kulikotokea mabomu wananchi wanajitakia, sehemu zile sio za kujengwa nyumba ila wanaotowa vibali vya kujengwa na wananchi wanaokubali ili wapate kujenga tu bila muundo mbinu ni wanamakosa huo ndio ukweli ila wote tunajuwa mafuriko yanaweza kumkuta mtu popote pale ila ujengaji wa ovyo Tanzania upingwe Usalama wa mazingira hakuna.
Asante kwa ujumbe wako. Tunakubaliana kuwa kuna aina fulani ya uzembe Tanzania ambayo husababisha hasara ya maafa haya ya mafuriko kuwa makubwa mno.
Post a Comment