Monday, October 3, 2016

Mkutano wa Africa Network


Wikiendi hii nilikuwa chuoni Denison, katika jimbo la Ohio, kuhudhuria mkutano wa Africa Network, mtandao wa vyuo vinavyoshughulikia masomo juu ya Afrika. Nimekuwa mwanabodi wa Africa Network tangu mwanzo, na nimeshuhudia historia yake hadi leo. Mtandao wa wanachama na washiriki wetu unaendelea kupanuka.

Picha zote zinazoonekana hapa nilipiga mimi, ambaye naonekana hapa kushoto.




Mikutano ya Africa Network ni fursa ya waalimu na watafiti kubadilishana mawazo na uzoefu katika taaluma na nyanja mbali mbali zinazohusu Afrika. Wikiendi hii, tulipata fursa ya kusikia na kujadili mada juu ya masuala kama uhifadhi na usambazaji wa kumbukumbu kidigitali, historia ya kale ya Afrika na umuhimu wake katika masomo juu ya Afrika, kuboresha viwango na ubora katika elimu ya juu, program za kupeleka wanafunzi Afrika.
Mkutano wetu huo ulijumlisha washiriki kutoka Marekani na nchi kadhaa za Afrika. Kwa ujumla wetu, tuna uzoefu wa utafiti katika nchi nyingi za Afrika, kama vile Ghana, Kenya, Msumbiji, Senegal, Tanzania, Uganda, Zambia, na Zimbabwe. Taaluma tunazowakilisha ni kama anthropolojia, uchumi, fasihi, historia, na lugha.




Nitaendelea kuandika kuhusu mkutano wa wikiendi hii, kwani ninazo kumbukumbu nyingi.

No comments:

Tangazo la Maongezi Yangu Books on Central, Faribault

Kwa miaka mingi, nimeongea na hadhira mbali mbali hasa kuhusu tofauti za tamaduni. Matangazo huandaliwa na kusambazwaa kabla ya mikutano. Ka...