![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhLsDSVVoL34_wM340ldpGOVtLt_xPeEWWION58pzUDYu5ShyZuYAI4L7zNo8FFvJQzFZ1AoTmNmqCyYcWspANcvvGc89biLHg0jK42CeuBZKocpq84UmUa0Mkv3FM-JiC1OFblwc2MVWA/s200/42498159_10204669304249359_615948428219777024_n.jpg)
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEj9N-PXa8aN-_lxw9W_ApGyb2JaHu2csyaK9UlWgaRW2iHitFxuGG0ve3GRBYaxMoyjDVEwFCz6AiAoAwPcJ-gDy5R6HBnFHoTauz_2CqdclYgkJnBgfmtTWD2awRgpfEmSkunqL_dxt5M/s200/42415436_10204669301289285_8172463062159196160_n.jpg)
Hapa kushoto ndio mwonekano wa kabati ambapo huwekwa vitabu vilivyopendekezwa na wahudumu wa duka. Kitabu changu kinaonekana hapo chini. Duka lolote la Barnes and Noble huwa na vitabu vingi sana. Ni kama maktaba. Kwa hiyo, kitabu kuuzwa humo si jambo la ajabu. Hakunaajabu yoyote kwa kitabu changu kuuzwa Barnes and Noble. Kama nilivyoandika juzi, kitab changu hich kimekuwepo kwenye mtandao wa Barnes and Noble kwa muda mrefu.
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiJf-TAsKt5VPBrTz7XOZmr54d4x_8rkMuX6AY2eErKFbp4CXeTfgs39obF2HNkwQj84UgEoP7Ys8dnV6eQ9ly9zfQCJFc0-DJxEJOaiNd4RHlAq_S_btKeyV3SzaRCigB6r6Ax4Rtbocw/s320/42540327_10204669290249009_8961432529911414784_n.jpg)
Kitu cha pekee ni uamuzi wa mhudumu wa duka kukipendekeza kwa wateja, kama inavyooneka hapa chini ya kitabu:
Short and sweet. A wonderful read about the differences between Africans and Americans. I feel wiser to the world after reading it.
Tafsiri yangu:
Kifupi na kitamu. Andiko la kupendeza ajabu kuhusu tofauti za tamaduni baina ya waAfrika na waMarekani. Najiona nimejiongezea werevu mbele ya dunia baada ya kukisoma.
Ninafurahi kwa sababu huyu mhudumu, mwenye uzoefu katika maktaba amesema hivyo. hudumu wa maktaba hapa Marekani ni msomaji wa vitabu. Anapopendekeza kitabu hawezi kupendekeza kiholela. Aanajua kuwa wadau wanaofika humo ni wa kila aina. Wengine ni wasomi waliobobea. Anaweka heshima yake rehani, kwani wadau wakinunua wakaona si kitabu bora, ataaibika yeye kabla ya mwandishi. Hiyo ni sababu ya wazi ya mimi kufurahi.
No comments:
Post a Comment