Sunday, May 12, 2019

Furaha ya Kujipatia Kitabu

Tarehe 26 hadi 28 Aprili, palifanyika maonesho ya vitabu Blaine, Minnesota, kama nilivyoelezea katika blogu hii. Nilishiriki, na kati ya watu waliokuja ni huyu binti ninayeonekana naye pichani.

Alifika kwenye maonesho tarehe 27, ila mimi sikuwepo. Tarehe 28 alifika tena na hapo ndipo nilipoambiwa kuwa huyu binti alishakuja akanunua kitabu cha Africans and Americans: Embracing Cultural Differences. Aliponiona alifurahi, akaniambia kuwa alitaka nisaini kitabu, lakini alikuwa amekiacha nyumbani. Nilisaini kitabu kingine nikampa. Hii ndio habari nyuma ya tabasamu la binti pichani.

Ninafurahi kuona vijana wenye mwamko wa kusoma vitabu. Huyu binti aliniambia kuwa anatoka Sudani ya Kusini. Alivutiwa na kitabı kwa sababu anaona utamaduni wa wazazi wake na yeye anakulia hapa Marekani. Hivi karibuni nimemwambia nitafurahi kusikia maoni yake kuhusu kitabu hiki.

No comments:

Tangazo la Maongezi Yangu Books on Central, Faribault

Kwa miaka mingi, nimeongea na hadhira mbali mbali hasa kuhusu tofauti za tamaduni. Matangazo huandaliwa na kusambazwaa kabla ya mikutano. Ka...