Friday, August 12, 2011

Kalenga Kwenye Makumbusho

Jana, pamoja na wanafunzi wangu, tulitembelea makumbusho ya Mkwawa, yaliyopo Kalenga, karibu na Iringa. Tulipata maelezo mengi ya historia ya wa-Hehe. Tulipata fursa ya kuangalia vitu mbali bali vilivyomo katika makumbusho hayo, kama vile silaha za jadi, zana za kilimo, vyombo vya nyumbani, picha, na maandishi. Kitu cha kukumbukwa zaidi ni fuvu la Chifu Mkwawa.

Hapo ni mahala muhimu kwa kwenda kujifunza historia sio tu ya wa-Hehe bali ya Tanzania. Kwa mfano, katika makumbusho haya kuna kuna zana za mawe za kale zilizopatikana Isimila.

Idara inayohusika na hifadhi ya makumbusho hayo inafanya kazi nzuri katika mazingira magumu. Hata hivi, hakuna sababu yoyote kwa nini Tanzania isiweke kipaumbele katika kuipa idara hii kila msaada unaohitajika. Umma wa wa-Tanzania unapaswa pia kuamka ili utambue umuhimu wa makumbusho kama haya. Haipendezi, kwa mfano, kuona watu wanajichukulia viwanja na kujenga nyumba katika maeneo ambayo ni ya kihistoria. Wa-Tanzania tujiulize: je, iwapo ukuta mkuu wa China ungekuwa katika nchi yetu, tungekuwa tumeutunza kama wanavyofanya wa-China? Naogopa kuwa kutokana na elimu duni, watu wangeng'oa mawe ya ukuta huo na kujengea nyumba.
Ikitunzwa vizuri na kutangazwa ipasavyo, hifadhi kama hii ya Kalenga ni hazina yenye mchango mkubwa katika elimu sio tu ya wa-Tanzania bali walimwengu kwa ujumla. Ni kivutio ambacho kinaweza kuchangia sana katika uchumi wa eneo hili.

3 comments:

Emmanuel said...

Hongera Prof. Ninapakumbuka sana hapo maana wakati nasoma Tosa ilikuwa karibu sana. Umeitembelea hapo mahali wakati nchi yetu inakosa viongozi wajasiri kama Mkwawa! Natumaini utawapelekea wengi maana ya hayo makumbusho

Kila la kheri katika safari zako

Emmanuel

John Mwaipopo said...

kila la heri katika safari zako za mafunzo. hatutaonana ukifika mbeya kwani sasa niko nje ya mji huo kwa shuguli zingine.

Mbele said...

Shukrani Ndugu Emmanuel. Nitajitahidi kuwajibika ipasavyo, kuhusu hao vijana.

Ndugu Mwaipopo, shukrani kwa ujumbe. Jioni hii ndio nimeingia Mbeya. Insh'Allah tutaonana wakati mwingine. Nitakuwepo hapa hadi tarehe 21.

Tangazo la Maongezi Yangu Books on Central, Faribault

Kwa miaka mingi, nimeongea na hadhira mbali mbali hasa kuhusu tofauti za tamaduni. Matangazo huandaliwa na kusambazwaa kabla ya mikutano. Ka...