Thursday, August 18, 2011

Niko Mbeya

Jana jioni nimeingia mjini Mbeya, nikitokea Njombe. Niko na wanafunzi kutoka Marekani, ambao hatimaye nitawapeleka Chuo Kikuu Dar es Salaam ambako watasoma kwa muhula mmoja.

Kwa vile ilikuwa ni usiku, sikuweza kuuona mji vizuri. Leo asubuhi nimeanza kutembelea maeneo ya mji, kama vile Mwanjelwa. Nategemea kupata fursa ya kuuona mji huu na pia sehemu zingine za mkoa wa Mbeya.

No comments:

Tangazo la Maongezi Yangu Books on Central, Faribault

Kwa miaka mingi, nimeongea na hadhira mbali mbali hasa kuhusu tofauti za tamaduni. Matangazo huandaliwa na kusambazwaa kabla ya mikutano. Ka...