Saturday, September 24, 2011

Kweli Blogu Inaweza Kuwa Shule

Baadhi yetu wanablogu tumewahi kutafakari na kujadili suala la blogu kama shule. Binafsi, nashukuru kuwa mara kwa mara napata ujumbe kutoka kwa wadau wanaosema wanajifunza kutokana na blogu zangu.

Leo kule Facebook kajitokeza mama mmoja mw-Arabu anayeishi Kuwait City. Kaniambia kuwa yeye ni mwalimu wa ki-Ingereza, na anafanya utafiti wa shahada ya juu kuhusu mwandishi J.M. Coetzee, hasa kitabu cha "Waiting for the Barbarians." Amesema kuwa amefurahi kuwa nilikubali kuwa rafiki yake Facebook na anangojea kwa hamu kupata ushauri wangu kuhusu tasnifu anayoandika. Ameendelea kusema kuwa katika kupitapita mtandaoni aliiona makala yangu kuhusu kitabu hiki. Makala yenyewe ni hii hapa.

Haya basi, mambo ya aina hii yanapotokea, kwa nini nisikiri kuwa blogu inaweza kuwa shule? Simaanishi kuwa taaluma yote husika inapatikana hapa kwenye blogu. Hata shule ni hivyo hivyo; haikuwezeshi kumaliza masomo, wala huwezi kuhitimu, ingawa walimwengu wanajidanganya na wanadanganyana kuwa wanahitimu. Shule inatoa dokezo na changamoto, na mwenye akili anafuatilia baada ya pale.

Ninaposema blogu inaweza kuwa shule nina maana hiyo hiyo, kwamba kile kinachowekwa katika blogu kinaweza kuwa dokezo na changamoto ya kuwawezesha walimwengu kutambua mtu unahusika na masuala gani na kisha wakafuatilia. Ndicho kilichotokea kwa huyu mama wa Kuwait City, na Insh'Allah nitafanya lolote niwezalo katika kumpa ushauri.

No comments:

Tangazo la Maongezi Yangu Books on Central, Faribault

Kwa miaka mingi, nimeongea na hadhira mbali mbali hasa kuhusu tofauti za tamaduni. Matangazo huandaliwa na kusambazwaa kabla ya mikutano. Ka...