Friday, September 30, 2011

Shule Niliyotembelea Madison

Jana asubuhi nilitoa mhadhara katika shule inayoonekana pichani hapa kushoto, ambayo iko mjini Madison, Wisconsin. Kama nilivyoandika kabla, mhadhara ulihusu yale niliyoandika katika kitabu cha Africans and Americans: Embracing Cutural Differences.

Wanafunzi yapata 150 walikuwepo darasani kunisikiliza. Mwalimu wao alikuwa amewapa vifungu vingi kutoka katika kitabu hicho wasome, na pia aliwapa masuali ambayo waliyatafakari na kuyajibu kabla ya ujio wangu. Walikuwa wamejiandaa vizuri. Ni wanafunzi makini, wenye duku duku ya kufahamu mambo, nami nilifurahi kupata fursa ya kuwahamasisha kuhusu kuzifahamu tamaduni mbali mbali, kwa kusoma, kujumuika na watu wa tamaduni hizo, na ikiwezekana, kwenda kwenye nchi mbali mbali, hasa katika programu za masomo kama hizo ninazoshughulika nazo.

Hii ni shule ya Kanisa Katoliki. Ilinikumbusha utoto na ujana wangu, nilivyosoma katika shule ya msingi na seminari za Kanisa Katoliki mkoani Ruvuma. Nakumbuka katika seminari kulikuwa na kauli mbiu iliyokuwa inahimizwa muda wote: "Ora et Labora." Huo ni usemi wa ki-Latini, na maana yake ni "Sala na Kazi." Tulifundishwa kuzingatia yote mawili, na kuwa kazi inahitaji kufanywa kwa dhamiri na uaminifu, ili kazi nayo tuione kama sala. Shule ya Edgewood ilinikumbusha mambo ya aina hiyo.

No comments:

Tangazo la Maongezi Yangu Books on Central, Faribault

Kwa miaka mingi, nimeongea na hadhira mbali mbali hasa kuhusu tofauti za tamaduni. Matangazo huandaliwa na kusambazwaa kabla ya mikutano. Ka...