Tuesday, January 10, 2012

Nimeenda Maktaba ya Southdale, Edina.

Leo nilienda mjini Edina, kwenye maktaba ya Southdale. Nilikwenda kukutana na mama mmoja m-Marekani Mweusi, ambaye ninamsaidia kuchapisha kitabu chake kwa kutumia tekinolojia ya uchapishaji mtandaoni, kama ninavyochapisha vitabu vyangu.

Niliposogea kwenye jengo hilo, niliona magari mengi yamepaki. Ni kama inavyokuwa kwenye sherehe nchini Tanzania.

Niliona watu wakiingia na kutoka, wakiwemo wazee. Hii ni kawaida hapa Marekani. Hapo mlangoni, nilipishana na wazee wawili wakitoka, mwanamme na mwanamke, wazee sana, na huyu mwanamme alikuwa anatembelea mkongojo. Pamoja na uzee wote huu, wanaona umuhimu wa kwenda maktaba. Humo ndani, kama kawaida, kulikuwa na watu wengi wakisoma, kuazima au kurudisha vitabu, na wengine kwenye kompyuta na kwenye sehemu za kusikilizia vitabu, maana siku hizi vitabu vinapatikana vikiwa vimerekodiwa katika kanda.

Ukiangalia maelezo ya maktaba hii Southdale, utaona kuwa wanavyoitumia maktaba hii inaendana vizuri na yale aliyoyawazia na kuyatamka Mwalimu Nyerere wakati anafungua maktaba ya Taifa Dar es Salaam, kama nilivyoandika hapa.

No comments:

Tangazo la Maongezi Yangu Books on Central, Faribault

Kwa miaka mingi, nimeongea na hadhira mbali mbali hasa kuhusu tofauti za tamaduni. Matangazo huandaliwa na kusambazwaa kabla ya mikutano. Ka...