Thursday, January 12, 2012

Nimerudi kutoka Chuoni Gustavus Adolphus

Leo nilienda Chuoni Gustavus Adolphus kutoa mhadhara katika darasa la Profesa Paschal Kyoore. Niliandika kuhusu habari hii hapa. Somo wanalosoma ni "African Tricksters." Wakati huu wanasoma kitabu changu cha Matengo Folktales, na niliona wanazo nakala.

Katika mhadhara wangu, uliodumu dakika 50, nilijikita katika kufafanua dhana mbali mbali zinazotumika katika utafiti na uchambuzi wa somo hili, ambazo chimbuko lake ni katika utafiti uliofanywa Ulaya, na jinsi dhana hizi zilivyopachikwa katika masimulizi ya sehemu zingine za dunia, kama vile Afrika. Nilihoji uhalali wa jambo hilo, ambalo tumelirithi na tunaliendeza.

Baada ya mhadhara wangu, tulikuwa na kipindi cha masuali, kilichodumu yapata dakika 40.

No comments:

Tangazo la Maongezi Yangu Books on Central, Faribault

Kwa miaka mingi, nimeongea na hadhira mbali mbali hasa kuhusu tofauti za tamaduni. Matangazo huandaliwa na kusambazwaa kabla ya mikutano. Ka...