Monday, July 23, 2012

Ziara Chuo Kikuu cha Dar es Salaam

Baada ya mizunguko yangu Songea, nimerejea Dar es Salaam jana jioni. Leo nilienda Chuo Kikuu cha Dar es Salaam. Nilionana na walimu na watafiki kadhaa, katika masomo ya uhandisi, :"Literature," na Kiswahili.

Nilitumia muda katika maktaba. Katika hifadhi ya "East Africana", niliangalia miswada kadhaa ya tungo za zamani za ki-Swahili. Halafu nilipita kwenye sehemu ya majarida ("Periodicals") na sehemu ya "Reference".

Kuna changamoto zinazoikabili maktaba hii, kama ilivyo kwa maktaba zote hapa nchini. Vinahitajika vitabu vipya na majarida. Hapo "Reference," niliona kwa mfano, nakala ya "MLA Handbook" iliyopo ni ya zamani, toleo la tatu. Itabidi safari ijayo niwaletee nakala ya toleo jipya. Nimewahi kuleta vitabu katika maktaba ile na wala sio jambo gumu. Wa-Tanzania tunaoishi nje au tunaosafiri nje, tungeweza kabisa kutoa mchango mkubwa kwa maktaba zetu kwa kuleta vitabu viwili vitatu. Sio jambo gumu, tukizingatia kuwa tuna utamaduni wa kuleta vipodozi au mizinga ya vinywaji vikali kama Jack Daniels.

Nilipokuwa katika taasisi ya Taaluma za Kiswahili, nilielezwa kuhusu mipango ya kuanzisha digirii ya juu katika fasihi.Niliambiwa kuwa wanahitaji nakala ya tasnifu yangu ya shahada ya udaktari, iitwayo "The Hero in the African Epic," ambayo niliiandika na kuitetea katika Chuo Kikuu cha Wisconsin-Madison. Nimeahidi kuwaletea, Insh/Allah.

Tena wamesema wana mipango ya kuanzisha mitihani ya ki-Swahili kama ile ya ki-Ingereza iitwayo TOEFL. Hii ni habari njema kabisa.

Katika idara ya Literature, ambapo nilifundisha kuanzia mwaka 1976, tuliongelea mambo kadhaa, likiwemo suala la wanafunzi tunaowaleta kutoka Marekani. Nilielezwa chagamoto za utaratibu uliiopo sasa, wa mihula mifupi, tofauti na zamani tulipokuwa tunafundisha somo kwa mwaka mzima.

No comments:

Tangazo la Maongezi Yangu Books on Central, Faribault

Kwa miaka mingi, nimeongea na hadhira mbali mbali hasa kuhusu tofauti za tamaduni. Matangazo huandaliwa na kusambazwaa kabla ya mikutano. Ka...